• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

DED IGUNGA AWAASA WATUMISHI KUENDELEZA MAADILI KAZINI

Tarehe iliyowekwa: March 6th, 2025

MKURUNGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Selwa Abdalla Hamid amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia Watumishi wengi wa kada ya afya hususan katika kipindi hichi ambacho Igunga inakua kwa kasi na vituo vya afya na zahanati zimejengwa za kutosha.


 Selwa ametoa shukran hizo wakati akiongea na Watumishi wa Kada hiyo katika ukumbi wa mikutano wa Hospitali ya Wilaya hiyo.


‘’Hakika kipekee ninamshukuru Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kutupa Watumishi wengi kwa sababu tulikua na uhitaji mkubwa hususan kwenye huduma za afya,’’ alisema.


Aidha, aliwataka watumishi hao kuendelea kufanya kazi kwa weledi wakizingatia miiko ya taaluma zao, kuepuka kuomba rushwa kwa wagonjwa, kutotumia lugha mbaya kwa wagonjwa ikiwemo kuingia kazini huku wakiwa katika hali ya ulevi.


Pia, aliwahakikishia kuwa Halmashauri itaendelea kuwathamini na kuwawezesha kupata stahiki zao kulingana na miongozo ya serikali.


‘’Ndugu zangu niendelee kuwakumbusha kuwa Halmashauri haitasita kuchukua hatua za kinidhamu kwa mtumishi yoyote atakaeonesha utovu wa nidhamu,’’ alikemea.


Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa wilaya hiyo, Hamis Hamis alisema Serikali imeboresha mifumo mbalimbali ya watumishi.


 ‘’Niwakumbushe Watumishi wenzangu tuitumie hii mifumo kwa sababu inatusaidia kugundua mapema kama kuna taarifa hazipo sahihi, hivyo kumtaarifu Mkurugenzi kwa barua kwa lengo la kuhakikisha taarifa zinakua sahihi,’’ alisema.


Kwa upande wa Mkuu wa Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Lucia Kafumu alisema katika wilaya hiyo walipangiwa watumishi 63 ambapo watumishi 61 walikwisha ripoti na wapo kwenye vituo wakiendelea kuwahumumia wananchi.


Akizungumzia kituo cha Afya Nanga ambacho baadhi ya majengo yake yamejengwa kwa fedha za Halmashauri hiyo milioni 400, Lucia aliweka wazi kuwa wamepeleka Daktari mmoja na Mtu wa Usingizi kwa lengo la kuanza kutoa huduma za upasuaji hivi karibuni.


Naye Afisa Muuguzi na Mtaalam wa Dawa za Usingizi na Ganzi wa Hospitali hiyo, Daud Mahenge alisema wamekubali kubadilika na kuendelea kuwa waadilifu katika kazi zao.

==== //// ==== ///// =====



Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa