• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

Tarehe iliyowekwa: May 10th, 2025

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoa wa Tabora, Bi. Selwa Abdalla Hamid amewapongeza Venyeviti wa Vijiji na Vitongoji walioshinda katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Novemba 27, 2024.

Bi. Selwa ametoa pongezi hizo wakati wa Mafunzo ya kuwajengea uwezo wenyeviti hao wakiwemo Watendaji wa Vijiji na Kata yaliofanyika Jumamosi Mei 10, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Maxwel mjini hapa.

Amewakumbusha wadhifa na madaraka waliopewa ni lazima wasimamie vema kwa lengo la kuhakikisha wanatimiza majukumu yao huku akiwaasa wanapokwama kutosita kurejea kwa viongozi wao kupata msaada.

‘’Ndugu zangu mimi Mkurugenzi wenu nitakua bega kwa bega kwa lengo la kuhakikisha maendeleo yanaendelea kuwafikia wananchi katika maeneo yao,’’ amesisitiza na kutoa wito:

‘’Nendeni mkalete mabadilko chanya ya kimaendeleo ikiwemo kusimamia miradi iliyopo katika maeneo yenu na kutoa taarifa mahali sahihi.’’

Katika hatua nyingi, Bi. Selwa amewasisitiza nidhamu ya fedha hususani zile za serikali kwa sababu zinamiongozo yake, hivyo wadumishe uadilifu na kuambatana na burasa na hekima wakati wanapotoa maamuzi bila ya kuvunja sheria, taratibu na kanuni.

Kwa upande wa Mratibu wa Mafunzo kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa, Scholastica Nyabweke ameeleza viongozi hao wako karibu na wananchi, hivyo wanaowajibu wa kuhakikisha miradi shirikishi ya maendeleo inasimamiwa ipasavyo kwa sababu serikali imekua ikitoa fedha nyingi.

Ameongeza kuwa dhamira ya serikali ni kuendelea kuhakikisha wananchi wa Igunga wananufaika na maendeleo, hivyo wakayatumie mafunzo haya kwa lengo la kuleta tija.

Naye Mwenyeketi wa Kijiji cha Isakamaliwa, Ntelezu Itinga ameshauri mamlaka husika kuwapatia nakala za mafunzo hayo kwa lengo la kuendelea kujikumbusha na kuwa na weledi kujiepusha na makosa.

Mafunzo hayo yamehusisha mada ya Sheria za Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Muundo, Majukumu na Madaraka ya Vijiji, Mitaa na Vitongoji, Uongozi na Utawala Bora, Uendeshaji wa Vikao na Mikutano katika Ngazi za Vijiji Mitaa na Vitongoji.

Aidha, mada zingine ni Uibuaji, Upangaji na Usimamizi wa Miradi Shirikishi ya Kijamii, Usimamizi wa Ununuzi, Usimamizi wa Ardhi na Udhibiti wa Uendeshaji Miji na Masuala Mtambuka.

==== //// ==== //// ==== //// ====





Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa