• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

DED IGUNGA AWATAKIA KHERI WATUMISHI KUSHIRIKI SHIMISEMITA JIJIJNI TANGA

Tarehe iliyowekwa: August 15th, 2025

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Bi. Selwa Abdalla Hamid amewaasa Watumishi wanaokwenda kushiriki michezo iliyoandaliwa na Shirikisho la Michezo Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) kufanya vema na kurudi na ushindi.


Aidha, amemshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaongezea bajeti jambo ambalo limepelekea yeye kuiwezesha timu ya Halmashauri kushiriki michezo hiyo kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa Halmashauri hiyo.


Akizungumza na Watumishi hao, leo Alhamisi Agosti 14, 2025, katika Ofisi ya Halmashauri hiyo, Bi. Selwa amesema ni wajibu kuendelea kumshukuru Mhe. Rais Dk. Samia kwa kuwawezesha bajeti iliyofanikisha jambo hili ambalo ni kwa mara yakwanza kushiriki tangu Halmashauri hiyo ilivyoanzishwa 1994.


‘’Ninafurahi mtakavyopepeprusha  bendera  ya Igunga huko jijini Tanga, hivyo jambo la msingi ni kushiriki vema hivyo jisikieni fahari na mkacheze kwa bidii,’’ amesema na kuongeza kuwa:


‘’Niwaombe mwende huko kama familia moja na kitu kimoja huku mkitanguliza mbele nidhamu na heshima.’’


 Amewataka kuheshimiana wao kwa wao na wale watakaokutana nao katika mashindano hayo huku akiwaasa kutoweka dosari ya jina la Halmashauri yao.


‘’Ninafurahi! leo mpo wachache lakini mwakani tutajitahidi bajeti iongezeke zaidi twende wengi kwa sababu michezo ni afya na nia ajira,’’ ameahidi.


Kwa upande wa Ofisa Michezo wa Halmashauri hiyo, Fadhili Kayange amemshukuru na kumpongeza Mkurugenzi huyo kwa kufanikisha jambo hilo kwa sababu ameandika historia mpya ya Halmashauri hiyo.

Naye Ofisa Utumishi wa Halmashauri Hiyo, Rahel Hagai amemuahidi Mkurugenzi huyo wataitambulisha vema Halmashauri hiyo.


‘’Tunakushukuru Mkurugenzi wetu Bi. Selwa Abdalla Hamid hakika kutupa kibali  na kutugharamikia ni jambo kubwa, tunasema asante sana!” ameshukuru Rahel.

========== ///////// ==========


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI MAJIMBO YA MANONGA NA IGUNGA AGAWA FOMU WANAOTARAJIA KUGOMBEA UBUNGE IGUNGA

    August 15, 2025
  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI MAJIMBO YA MANONGA NA IGUNGA AGAWA FOMU WANAOTARAJIA KUGOMBEA UBUNGE

    August 15, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKIA KHERI WATUMISHI KUSHIRIKI SHIMISEMITA JIJIJNI TANGA

    August 15, 2025
  • WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA KATA WATAKIWA KUTUMIA KANUNI, SHERIA, TARATIBU NA MIONGOZO KUFANIKISHA UCHAGUZI MKUU 2025

    August 05, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa