• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

Harambee Shule ya Sekondari Choma

Tarehe iliyowekwa: December 2nd, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mh.John Gabriel Mwaipopo amekuwa Mgeni Rasmi katika Harambee ya uchangiaji wa Ujenzi wa Vyumba Vitano vya madarasa katika Shule ya Sekondari Choma iliyopo Tarafa ya Manonga Kata ya Choma. Akiongea na wananchi pamoja na Wageni waalikwa Mgeni rasmi alisema “Elimu ndiyo itakayo wakoomboa na ndio urithi wa watoto wetu kwa kuwa tumeshiriki kuwaleta hapa Duniani ni wajibu wetu kuwalea na kuwatunza  ikiwa ni pamoja na kusaidiana na Serikali yetu ya Jamuhri ya Muungano wa Tanzania kuimalisha miundombinu hasa madarasa”

Pia aliwaeleza wananchi kila Serikali inakuwa na vipaumbele hivyo ni wajibu wetu kama watanzania na watu wa Choma na   Igunga kwa ujumla kuchangia maendeleo.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Choma Mwl.Richard  Rutandula  akisoma taarifa fupi ya Shule ambayo ilionyesha mahitaji Makubwa ya shule  hiyo alisema “ Ndg Mgeni Rasmi Shule ya Sekondari Choma ilianzishwa rasmi mwezi Mei, 2006 ikiwa na Vyumba vinne vya Madarasa tu, ni shule ambayo ujenzi wake sambamba na nguvu za halmashauri ya Igunga , Serikali Kuu pia nguvu ya wanannchi wa Kata ya Choma yenye Vijiji mama vitatu ambavyo ni Choma, Chibiso na Bulangamilwa”.

Mkuu wa Shule aliendelea kusema shule kwa ujumla wake inamapungufu mengi katiak maeneo mbalimbali kama vile Vyumba vya Madarasa mahitaji 17 yaliyopo 08, pungufu 09, Nyumba za waalimu mahitaji 14, zilizopo 03, Mapungufu 11, Mabweni Mahitaji 05, Zilizopo 01, pungufu 04, Maabara, Vyoo Mahitaji Matundu 30, vilivyopo 06, Mahitaji 24, pia  madawati/Meza  Mahitaji 679,yaliyopo 446, Mapungufu 233.

Hivyo aliendelea kutoa mchanganuo wa makisio ya ujenzi wa Vyumba hivyo vitano vya madarasa ambapo makisio ya gharama zote za ujenzi na ukamilishaji wa Vyumba hivyo ni Tsh.23, 823,700.00 (Shilingi milioni ishirini na mbili laki nane ishirini na tatu elfu mia saba tu). 

Mh. Peter Onesmo Maloda Diwani Kata ya Choma na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Igunga ambaye ndiye aliyekuwa mwenyeji wa Harambee hiyo aliongozana na Mh.Williamu Wales Jomanga Mwenyekiti halmashauri ya Mji Nzega,

Mkurugenzi Mtendaji (W) Halmashauri ya Igunga Bw.Revocatus L.Kuuli pamoja na Afisa Elimu Sekondari Bw.Aloyce Kaziyareli walikuwepo katika harambee hiyo ambapo waliwawakiisha wakuu wa Idara na Vitengo. Pia Afisa Tarafa ya Manoga Bi.Maltha L.Tevely aliongozana na baadhi ya Watendaji wa Kata na Vijiji pamoja na viongozi wa taasisi mbalimbali zikiwemo za kidini.

 

Mgeni rasmi Mh.John Gabriel Mwaipopo (Mkuu wa Wilaya ya Igunga) akiongoza harambee hiyo aliweza kupata pesa taslimu kiasi cha (Tsh.230,000.00) shilingi laki mbili elfu thelethini tu, pamoja na ahadi (Tsh.2,975,000.00) shilingi milioni mbili laki tisa sabini na tano tu. Simenti  mifuko 113, Bati bandali Moja, Nondo 04,Mchanga gari moja vyote vikiwa na jumla ya (Tsh.5,420,000.00) shilingi milioni tano laki nne ishirini elfu tu.

 

Mh.Mgeni rasmi aliwaomba na kuwaagiza  Kamati ya shule na Mh.Diwani wa kata ya Choma Mh.Peter Onesmo Maloda ambaye ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga waendelee kuwahimiza wananchi  kuchangia ujenzi huo ili wanafunzi waweze kupata madarasa ya kujifunzia.


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa