• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

Hongera Mwayunge Sekondari Kwa Ufaulu Kidato cha Nne 2017

Tarehe iliyowekwa: January 10th, 2019

Mkuu wa Shule Mwayunge Sekondari mwalimu Amithayori R.Nehemia, amefurahi kuwa miongoni mwa shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2017, Wilayani Igunga alipokuwa anakabidhiwa tuzo ya Most Improved School (Shule iliyoongeza ufaulu kwa kiwango cha juu) katika ofisi za idara ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Igunga jana tarehe 09.01.2019.

Shule ya Sekondari Mwayunge imepata tuzo hiyo, miongoni mwa shule mbili nyingine ambazo zinazofanya vizuri kwa miaka miwili mfululizo ambazo ni  Umoja Sekondari na St. Thomas Sekondari zilizopata Tuzo ya Shule zinazofanya vizuri sana (Best Performing School) hapa nchini Tanzania.

“Mwayunge Sekondari ilianzishwa mwaka 2011, ikiwa na wanafunzi 82 wa kiume 39 wa kike 43 ambao walihitimu kidato cha nne mwaka 2014. wa kiume 23 wa kike 9 na hakuna aliyeendelea na masoma ya elimu ya kidato cha tano, Mwayunge ina jumla ya walimu 22 wa kiume 12 na wa kike 10” ameongeza Mwl  Nehemia Mkuu wa Shule.

Mwaka 2015 Shule ya Sekondari Mwayunge ilifanya vibaya katika mitihani yake ya kidato cha nne, kwa ushirikiano wa walimu na Idara ya Elimu Sekondari Wilaya ya Igunga. Mwaka 2016 Mwayunge Sekondari ilifanya vizuri na kupongezwa kwa kupatiwa cheti pamoja na fedha tasilimu Tsh.2,000,000.00 toka Wizara ya Elimu Sayansi naTeknolojia.

 “Shule ya Sekondari Mwayunge imeendelea kuongeza bidii katika ufundishaji na ujifunzaji, ambapo kwa mwaka 2017 iliongeza ufaulu kwa kiwango cha juu,(Most improved School) ambapo tumepokea tuzo hii tukiwa miongoni mwa shule zilizoongeza ufaulu  nchini kwa mwaka 2017”ameongeza Mwalimu Nehemia Mkuu wa Shule.

“Nampongeza Mkuu wa Shule na Walimu wote kwa kuongeza ufaulu,na kuwashauri waendelee kuongeza bidii ili ufaulu kwa mitihani ya kitaifa na mitihani ya ndani uongezeke zaidi pia  kuwaimarisha wanafunzi kimaarifa na kuendelea  kuiletea sifa Shule,  idara ya Elimu Sekondari pamoja na halmashauri kwa ujumla”ameongeza Kaimu Afisa Elimu Sekondari Rashid Bundallah.

Mwayunge Sekondari ina Jumla ya wanafunzi 415, na inategemea kupoke wanafunzi 100 wa kidato cha kwanza mwaka 2019 ambao watafanya shule kuwa na wanafunzi 515. Kidato cha nne 2019 ni wanafunzi 93 wa kiume 41  na wa kike 52 matarajio ya walimu na mkuu wa shule  ni kupeleka wanafunzi 35 kidato cha tano kwa 2020.

Shule inamafanikio iliyoyapata japo palipo na mafanikio hapakosi changamoto, Mwayunge Sekondari ina mapungufu ya nyumba za walimu 22, Jengo la Utawala pamoja na maabara zote tatu maabara ya Fizikia, Biolojia na Kemia.

Mkuu wa shule ameipongeza Serikali ya awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  kwa kuwezesha Shule kupata fedha za Elimu bure pamoja na kushirikishwa kufanya maamuzi katika ngazi za shule. Amewashukuru walimu wote kwa kuendelea kumpa ushirikiano katika kuendelea kuimalisha Mwanyunge Sekondari na halmashauri ya Wilaya ya Igunga.

Imetolewa na

Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO

Halmashauri ya Wilaya ya Igunga.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa