• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

IGUNGA KINARA MRADI HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI NCHINI

Tarehe iliyowekwa: February 12th, 2025

UTEKELEZAJI na usimamizi sahihi wa Mradi wa Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (SRWSS) umeiwezesha Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora kushika nafasi ya kwanza kati ya Halmashauri zote nchini.

Aidha, hatua hiyo imeiwezesha Halmashauri hiyo kupata fedha za kutekeleza miradi mbalimbali katika Zahanati ya Mwamapuli, Matinje na Mwajinjama awamu ya kwanza huku awamu yapili ikitekeleza Dispensari ya Nguriti, Utuja, Mgazi, Itumba na Ziba.

Akizungumza katika kikao kazi kilichofanya Jumamosi Februari 08, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo, Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Sauda Mtondoo aliipogeza timu inayoongozwa na Mganga Mkuu wakiwemo wote walioshiriki katika utekelezaji wa mradi huo ambao ulipelekea kuvuna takribani sh. bilioni tatu, hivyo  Halmashauri hiyo kushika nafasi ya kwanaza kitaifa.

‘’Hongereni ! haikua kazi ndogo, ilikua kazi kubwa, hivyo mwenendo huo umetufanya kukutana leo kuweka mikakati ya kuvuna zaidi kuliko msimu uliopita  kwa sababu ari tuliyonayo ya umoja tunaweza,’’ alisema Mhe. DC Sauda na kuongeza kuwa:

‘’Kila mmoja kwa nafasi yake akasimame vema hususan waliopokea fedha awamu ya kwanza kwa sababu wamebeba dhamana ya aidha kuwahi au kuchelewa kupata fedha za awamu ya pili.’’

Aliwataka Wajumbe hao kuisemea miradi hiyo kwa wananchi kwa lengo la kuhakikisha wanaifahamu kwa sababu wao ni semhemu ya usimamimizi na utekelezaji wa miradi hiyo.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Lucas Bugota aliendelea kuipongza Idara ya Mganga Mkuu kwa kuwaheshimisha wananchi wa Igunga kufuatia Halmashauri hiyo kuongoza Kitaifa.

‘’Ninawapongeza sana, kwa kweli ni jambo kumba, Wilaya na Halmashauri ziko ngapi Tanzania nzima lakini imeonekana Igunga,’’ alipongeza Bugota.

Alieleza kuwa miradi hiyo inatekelezwa ngazi ya kijiji na Kata, hivyo Madiwani na Watendaji wa Kata ndio viongozi wakuu wasimamie fedha za serikali mpaka miradi inapokua imekamilika.

‘’Nendeni mkasimamie miradi ikamilike kwa wakati kwa sababu Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameleta fedha nyingi amabazo ni za kutusaidia sisi,’’ alisema.

Kwa upande wa Mkuu wa Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Lucia Kafumu alimshukuru Mkuu huyo wa Wilaya kwa kuungana na watalaamu hao katika kikao hicho kwa sababu wanaamini maneno yake ni tiba kwao na yanawapa nguvu yakwenda kuwajibika zaidi.

Naye Afisa Afya wa Wilaya hiyo, Muhoja Lubeja alisema utekelezaji wa Mradi huo unahusisha Idara ya Elimu, Afya na Maji huku kwa upande wa Afya mradi huo unajishughulisha na uhamasishaji wa vyoo ngazi ya kaya na jamii.

Alidokeza kuwa awamu ya kwanza walipokea sh. milioni 218 kati ya Sh. Milioni 727 ambazo wanatarajia kuzipokea awamu zinayofuata.

Aliweka wazi chanzo cha fedha hizo ni baada ya kufanyika uhakiki wa masuala ya afya na usafi wa mazingira ngazi ya kaya na vituo vilikidhi vigezo vilivyowekwa na wafadhili Benki ya Dunia kwa kushirikiana na serikali.

==== //// ==== //// ==== ///// =====




Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa