• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

IGUNGA MATUMIZI YA KIDIJITALI YASHIKA KASI

Tarehe iliyowekwa: January 29th, 2026

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Mhe. Shabani Hemedi ameliongoza Baraza la Madiwani kumpongeza Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuiletea fedha nyingi zinazotekeleza miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.


Mhe. Hemedi ametoa pongezi hizo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2025 hadi 2026 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo mjini Igunga januari 28, 2026.


Ameliomba Baraza hilo kutowavumilia watumishi watakaoshindwa kusimamia miradi iliyoletewa fedha na Rais Dk. Samia kusimamia miradi  ikamilike kwa wakati.


"Waheshimiwa Madiwani itakapofika hatua hiyo, niwaombe mniunge mkono,  mtumishi wa namna hiyo hatakua na sifa ya kufanya kazi katika Halmashauri hii," amesisitiza.


Akizungumzia Vishikwambi alivyogawa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Bi. Selwa Hamid, Mhe

 Hemedi amempongeza Mkurugenzi huyo huku akiwataka Madiwani wakavitunze vishikwambi.


Aidha, amesema hatua hiyo ni mwendelezo wa kumuunga mkono Mhe. Rais Dk. Samia ambae ameadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kupanda mti jambo ambalo linatoa tafsiri yakutokata miti kutengenezea karatasi.


Katika hatua nyingine, amewahimiza Madiwani kuwahamasisha wazazi na walezi katika kata zao kuhakikisha watoto na wanafunzi wanaotakiwa kuwa shule wanapelekwa shule kwa sababu muda ndio huu.


Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Bi. Selwa Hamid amesema ametimiza ahadi ya kugawa vishikwambi kwa Madiwani 46 kwa lengo la kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dk. Samia kuhusu matumizi ya kidijitali.


"Leo tunaungana na Mhe. Rais Dk. Samia katika matumizi ya kidijitali, hivyo tunaanza kutumia vishikwambi katika vikao vyetu na kuepukana na matumizi ya karatasi," amesema.


Aidha, amesena wamepokea maelekezo yote na watayafanyia kazi.


Naye Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Halmashauri hiyo, Ndug. Hamisi Hamisi amewaomba viongozi hao kuvitunza vishikwambi hivyo kwa sababu ni mali ya serikali.

================

Matangazo

  • WAHI FURSA ZA UWEKEZAJI IGUNGA September 25, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA October 28, 2025
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • IGUNGA MATUMIZI YA KIDIJITALI YASHIKA KASI

    January 29, 2026
  • MAFUNZO YAWAONGEZEA UJUZI NA UMAKINI MADIWANI NA WATAALAMU KUIONGOZA HALMASHAURI

    January 24, 2026
  • MWENYEKITI MTEULE ATOA DIRA KUIONGZA HALMASHURI KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO

    December 05, 2025
  • HAMISI ANENA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU YAMEKAMILIKA IGUNGA

    October 27, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa