• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

KUJIKWAMUA KUTOKA KWENYE UMASIKINI INAWEZEKANA WANANCHI TEKELEZENI MIKAKATI STAHIKI

Tarehe iliyowekwa: February 2nd, 2025

MKUU wa Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Mhe. Sauda Mtondoo amemshukuru na kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kupambana kuhakikisha mambo yanayowagusa Watanzania wakiwemo wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) anatafuta fedha kwa lengo la kuhakikisha mpango huo unaendelea.


Mhe. Sauda ametoa shukran na pongezi hizo Ijumaa Januari 31, 2025 wakati akiongea na Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) kijiji cha Igumila Kata ya Ziba wilayani hapa.


Aidha, aliweka wazi kuwa dhamira ya serikali ni kuona Wananchi wanainuka kutoka walipokua na kupiga hatua zaidi, hivyo wajitafakari na kuuchukia umaskini kwa kuwa baadhi yao wamekuwa wakipokea fedha kwa muda mrefu.


‘’Ndugu zangu hichi kiasi kidogo mnachokipata endeleeni kuweka mikakati ya kuhakikisha mnaondokana na umaskini, ninawaomba msimame imara kwa lengo la kutoka katika hali ya umaskini kwa sababu inawezekana,’’ alisistiza.


Alifafanua kuwa serikali inaendelea kuwajali, hivyo wanaweza kulima na kupata mazao ambayo wanaweza kuyatumia kwa chakula na mengine kuuza, kufuga kuku au mbuzi kisha wakawavuna na kuwauza kwa lengo la kujiongezea kipato.


Alisema ni lazima wawe na dhamira ya dhati ya kuuchukia umaskini kwa kuanzisha hata biashara ndogondogo ambapo wataweza kuendelea.


‘’ Ninawahamasisha ndugu nzangu kuuondoa umaskini licha yakuwa sio rahisi lakini inahitaji moyo na ujasiri na kujituma,’’ alisema.


Kwa upande wa Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Elizabeth Rwegasira aliwataka wasimamizi wa miradi inayotekelezwa kupitia mpango huo kuongeza usimamizi wa karibu kwenye miradi hiyo kwa lengo la kuhakikisha wanapata matokeo ya kudumu.


Awali akiwasilisha taarifa fupi mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya kwa niaba ya Wanufaika wa TASAF Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Igumila, Jackrine Gibe alisema kijiji hicho kinatekeleza afua ya Uhawilishaji wa Fedha (CCT) na Miradi ya Ajira za Muda (PWP).


Aliongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2024 hadi 2025 walipokea fedha sh. milioni 15.072 kwa walengwa 144 hivyo kufanikiwa kujikwamua kutoka kwenye hali ya umaskini uliokithiri.






Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa