• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

MAADHIMISHO YA SIKU YA FAMILIA MEI 16 2023

Tarehe iliyowekwa: May 16th, 2023

 

 Familia ni chanzo cha jamii  yoyote Duniani  kwa kuwa kila mtu  amezaliwa na amekulia katika Taasisi hii  muhimu katika Jamii. Familia inaundwa na Mume,Mke na Watoto na katika utamaduni wetu Ndugu wakaribu wanakuwa sehemu ya familia.Majukumu ya Familia ni pamoja na kutoa huduma muhimu zikiwemo mahitaji ya Watoto na Familia,Ulinzi na Mawasiliano.

Kauli mbiu ya siku ya Kimataifa  ya familia Duniani kwa mwaka huu  2023 ni “Imarisha  Maadili na Upendo kwa Familia Imara”.Kauli mbiu hii  inatumika kuwakumbusha  nyinyi wazazi na walezi juu ya umuhimu  wa maadili mema na upendo miongoni mwa wanafamilia. Aidha  inawakumbusha wanafamilia  umuhimu wakuzingatia Maadili mema ya Kitanzania katika malezi na makuzi ya watoto wetu.Pia  kauli mbiu hii inasisitiza upendo ili kuepusha migogoro isiyo   ya lazima  inayopelekea familia nyingi kusambaratika  na kuacha watoto  bila uangalizi wapamoja hivyo kukosa huduma muhimu.

Maadhimisho haya yanawakumbusha wazazi  na walezi wajibu wenu wa msingi  katika malezi ya watoto na familia hasa akina baba wajibu wenu kama wazazi au walezi kwa watoto  katika maeneo makuu matatu ya msingi

  • Kumjali mtoto katika mahitaji ya msingi
  • Kumlinda mtoto dhidi ya ukatili
  • Kuzungumza na mtoto mara kwa mara ili kufahamu changamoto zinazomkabili na maendeleo yake kwa ujumla.

Pamoja na jitihada za Serikali katika kuhimiza maadili mema  na upendo  katika familia zetu  bado kunamatukio mengi ya ukatili wa watoto na wanawake yanayoshuhudiwa  katika ngazi ya familia  na katika jamii.Miongoni mwa matukio hayo ni pamoja na:-

  • Ubakaji
  • Ulawiti
  • Mimba za utotoni

Tafiti nyingi za ukatili dhidi ya watoto zinaonyesha kuwa ukatili wa watoto unafanyika zaidi nyumbani kwa asilimia 60 na shuleni kw asilimia 40 na wanaofanya ukatili zaidi ni ndugu na jamaa wa karibu na familia husika.Changamoto kubwa katika kukabiliana na ukatili  dhidi ya watoto  unatokana na ukimya wa wazazi na walezi katika kutoa taarifa za vitendo vya ukatili vinavyofanyika ndani ya familia  kwasababu tofautitofauti zikiwemo:-

Kuepuka hatua za kisheria  dhidi ya mkosaji,mila na desturi, kuwepo kwa Imani potofu zenye madhara  zinazotekelezwa  katika baadhi ya familia, uelewa mdogo kuhusu malezi chanya na mawasiliano duni miongoni mwa wanafamilia.Hali hii inapelekea watoto wengi  kujiingiza kwenye vitendo visivyofaa katika jamii  ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa utoro shuleni ,kuongezeka kwa vitendo vya ukatili na maambukizi ya VVU.

Ili kufikia lengo  la kuwa na familia imara  na zenye upendo wazazi na walezi mnatakiwa kutimiza wajibu wenu  kwa kuhakikisha  kuwa huduma  za muhimu  kwa watoto wenu zinatimizwa ikiwa ni pamoja na :-

  • Huduma za Afya  kwa kuwakatia  BIMA za iCHIF  watoto wenu.
  • Kuwapatia mahitaji ya shule  ikiwa ni pamoja na sare,vifaa vya shule  pamoja na mchango wa chakula shuleni.
  • Lishe bora na ulinzi wa mtoto nyumbani na shuleni.
  • Kutoa taarifa kuhusu vitendo vya ukatili wanaofanyiwa watoto katika familia zetu bila kujali ukatili huo umefanywa na ndugu au jamaa wakaribu kwa vyombo husika.
  • Kutoa haki na huduma sawa za  malezi  kwa watoto wote  bila kujali jinsia.

 

Ndugu Wananchi, Sisi sote tunatakiwa kushikamana katika kujenga  familia zenye maelewano yakutosha  na  yenye upendo kwani ndio msingi wa uzalishaji  mali utakao  wawezesha  kutoa  huduma  za msingi kwa watoto wetu na  kufuatilia  maendeleo yao  katika  makuzi, maadili na masomo yao shuleni.

 Familia  bora   zinatakiwa  kuwalea watotot wakiume  na wakike  kwa usawa  kwani wote  wanamchango  ulio sawa kwa maendeleo ya Taifa.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa