• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

MAFUNZO YAWAONGEZEA UJUZI NA UMAKINI MADIWANI NA WATAALAMU KUIONGOZA HALMASHAURI

Tarehe iliyowekwa: January 24th, 2026

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Mhe. Shabani Hemedi amewashukuru na kuwapongeza wakufunzi kwa kuwaelimisha mambo mengi kuhusu kuendesha Halmashauri kwa tija.


Mhe. Shabani ametoa shukran na pongezi hizo leo, Ijumaa Januari 23, 2026 wakati wakuhitimisha mafunzo kutoka kwa wakufunzi wa TAMISEMI na Hombolo tawi la Shinyanga yaliyofanyika katika ukumibi wa Halmashauri hiyo mjini hapa.


Kwa upande wa Meneja Rasilimaliwatu wa  Chuo cha Serikali za Mitaa Kampasi ya Shinyanga, Michael Boniface  amewaomba Madiwani na Wataalamu hao, kuelewa Wataalam wa Chuo hicho wapo tayari kuendelea kutoa mafunzo bure inapohitajika kwa sababu ndio maelekezo ya Mkuu wa Chuo hicho.


Aidha, ameongeza kuwa wanapokua na Watumishi ajira mpya na hawajapata mafunzo elekezi (orientation) wawape  mwaliko watakuja  kutoa mafunzo  hayo.


Katika hatua nyingine, ametoa wito kwa watumishi hao kujiandaa kustafu tangu siku ya kwanza walioanza kazi kwa kuanza kujenga kidogo kidogo kwa lengo la kujiepusha kushangaa wakati wa kustafu unapofika.


"Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio mema kazini, viongozi na wafanya kazi lazima wote tuwe na nidhamu, migogoro na migongano ya kazini ni ukosefu wa nidhamu," amesisitiza.


Kwa upande wa Mkufunzi kutoka Chuo hicho  katika tawi hilo, Lenatha Mwangesi  amewaeleza Madiwani ni wajibu wao kutumia ujuzi na vipawa vyao kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa lengo la kuhakikisha mipango mingi ya serikali ya kuwaletea wananchi maendeleo inatimia.


Akizungumza katika mafunzo hayo, Diwani wa Kata ya Isakamaliwa, Maganga Daud amewaomba wakufunzi hao kulifikisha kwa viongozi wa kitaifa kuhusu posho za Madiwani ziongezeke huku akiwaomba wabunge wawatetee bungeni na lisiwe swala la mchakato kwa sababu limekua la muda mrefu.

================////////////////



Matangazo

  • WAHI FURSA ZA UWEKEZAJI IGUNGA September 25, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA October 28, 2025
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YAWAONGEZEA UJUZI NA UMAKINI MADIWANI NA WATAALAMU KUIONGOZA HALMASHAURI

    January 24, 2026
  • MWENYEKITI MTEULE ATOA DIRA KUIONGZA HALMASHURI KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO

    December 05, 2025
  • HAMISI ANENA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU YAMEKAMILIKA IGUNGA

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI UCHAGUZI MKUU NGAZI YA VITUO WAKO TAYARI

    October 27, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa