• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

MENEJIMENTI YAAHIDI KUENDELEA KUIPAISHA IGUNGA KATIKA KILA SEKTA

Tarehe iliyowekwa: September 13th, 2025

TIMU ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, imefanya ziara fupi Jijini Mwanza kwa lengo la kufanya utalii mdogo wa ndani huku ikifanya tathimini ya utekelezaji wa majukumu yake mbalimbali ikiwemo kusimamia kwa ufanisi mkubwa miradi ya maendeleo inayoendelea kutoa huduma kwa wananchi.


Timu hiyo imefanya tathmini yake hivi karibuni baada ya kufanya vyema katika kila sekta mbalimbali ndani ya mwaka wa fedha 2024/2025 huku ikiahidi na kuweka mikakati thabiti na imara ya kuendelea kufanya kazi zake kwa bidii na uweledi mkubwa katika mwaka wa fedha  2025/2026.


Akizungumza na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri hiyo, Bi. Selwa Abdalla Hamid amewashukuru na kuwapongeza viongozi hao kwa kuendelea kuipaisha Igunga.


Amedokeza kwa upande wa Fedha na Uhasibu, Halmashauri hiyo imepata hati safi mfululizo kuanzia mwaka 2021 hadi 2023 huku ikikusanya mapato na kuvuka lengo kwa asilimia zaidi ya 103 kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025.


Aidha, akizungumzia kuhusu miradi, Bi. Selwa amewaka wazi katika mwaka huo wilaya hiyo ilipokea takribani sh. 115.5 bilioni kutekeleza miradi ya maendeleo.


"Hakika tunaendelea kumshukuru Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutupatia fedha nyingi  ambazo zimejenga miundombinu mbalimbali  ikiwewemo kuboresha hospitali yetu ya wilaya, zahanati na vituo vya afya," ameshukuru na kuongeza kuwa:



"Tumeboresha Miundombinu ya shule ikiwemo ujenzi wa shule mbili mpya za sekondari, ujenzi wa nyumba za maafisa ugani ili waweze kusimamia fani Yao kikamilifu kwenye sekta ya kilimo ndani ya kata zetu. Na Majengo yote yamekamilika na kuanza kutoa huduma, Hongerenii sana."


Pia, amesema Halmashauri imefanikiwa kutoa mikopo itokonayo na asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika kipindi hicho, kwa zaidi ya Tsh. 808.557 milioni kwa vikundi 65.


Akizungumzia Mpango wa kunusuru Kaya Masikini (TASAF), Bi. Selwa amebainisha walengwa 10,557 kutoka katika vijiji 119 na maeneo matano ya Mamlaka ya Mji Mdogo wamenufaika.


Amsema Halmashauri hiyo ilipokea Tsh. 14.771 bilioni zilitolewa kwa walengwa hao ambao waliibua miradi 80 ya kutoa ajira za muda.


"Wametekeleza miradi 59 ya barabara, visima sita, mabwawa, kivuko na mradi wa miti kwa asilimia 100," amedokeza.


Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa idara na vitengo, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri hiyo,  John Tesha amemuahidi Mkurugenzi huyo kuongeza ari na kasi ya kufanya kazi ili Halmashauri hiyo iendelee kujivunia utendaji wao wa kazi na kuweza kutoa matokeo chanya zaidi katika mwaka wa Fedha 2025/2026.


=================




Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MENEJIMENTI YAAHIDI KUENDELEA KUIPAISHA IGUNGA KATIKA KILA SEKTA

    September 13, 2025
  • MGAMBO WAASWA KUENDELEA KUWA WAZALENDO, WAADILIFU NA WAAMINIFU KWA TAIFA

    August 29, 2025
  • WAGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MANONGA NA IGUNGA KUPITIA CCM WAREJESHA FOMU KWA WAKATI

    August 27, 2025
  • WACHIMBAJI MADINI IGURUBI WAPEWA ELIMU KUHUSU TOZO ZA HALMASHAURI

    August 27, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa