• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

MHE. DC SAUDA MTONDOO AWAKUMBUSHA WANAWAKE KUENDELEA KUTUNZA, KULINDA NA KULEA FAMILIA

Tarehe iliyowekwa: March 6th, 2025

MKUU wa Wilaya ya Igunga mkoa wa Tabora, Sauda Mtondoo amewataka wanawake kufahamu pamoja na juhudi za kuendelea kupambania usawa, haki na uwezeshaji wanalo jukumu la msingi la  kulea, kutunza na kulinda familia.


Aidha, wanawake wanayo kazi ya kufanya kwa lengo la kuimarisha haki sawa na wanaume katika nyanja mbalimbali za maisha.


DC Sauda ameyasema hayo jana  katika Kongamano la Wanawake lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo mjini hapa.



Aliweka wazi kuwa katika suala la kutoa maamuzi, kumiliki ardhi na mirathi katika zile jamii ambazo zinaona Wanawake hawana haki ya kutoa maamuzi, kumiliki ardhi na mirathi.


‘’Tuendelee kutafakari kuimarisha haki na usawa katika nyanja ya uongozi na kutoa maamuzi hasa katika kipindi hichi ambacho Tanzania inapigiwa mfano kwa sababu inaongozwa na Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ’’ alisema.


Aidha, alieleza kuwa Wanawake wanapambana katika kujenga uchumi wa mtu mmoja mmoja, familia na Taifa kwa ujumla huku akiwaasa kutosahau kulea na kutunza familia zao.


Aliongeza kuwa Mwananke akisimama imara basi familia itasimama vizuri lakini akitetereka na familia itayumba yumba, hivyo wanatafuta na kupambana kwa lengo la familia, ni vema wajue mwenendo wa watoto na waume wao.


‘’ Hivi sasa kunachangamoto kubwa katika malezi na makuzi ya watoto wetu kwa kuingia kwenye makundi mabaya, wanawake ndio nguzo za familia, hivyo tusimame imara kuhakikisha malezi na makuzi ya watoto wetu yako vizuri,’’ alisema.


Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Selwa Abdalla Hamid aliwakumbusha waandaaji wa Kongamano hilo kuhakikisha Kongamano lijalo Wanaume nao wanakuwepo kwa lengo la kuona nguvu ya Wanawake katika Halmashauri hiyo.


Alisema wanapeleka shukrani zao  kwa Rias Dk. Samia kwa sababu amewachagua wao akiwaamini wanaweza kuongoza Wilaya ya Igunga kwa ushirikiano walionao.


‘’ Tunae Rais wetu ambae ni Mwanamke hivyo tunaweza kufanya chochote na popote ikiwemo kuwa Makamu wa Rais Mwanamke au Waziri Mkuu,’’ alisema na kuongeza kuwa:


‘’ Tunaweza kuleta mabadiliko, hivyo tuendelee kufanya kazi kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya kwa sababu tunauwezo mkubwa, tuendelee kujiamini na kuonesha umuhimu wetu.’’


Kongamano la Wanawake limefanyi ikiwa ni maandilizi ya kuelekea kilele cha maadhimisho hayo yatakayofanyika kimkoa Nzega Mji ifikapo Machi 08, 2025.

=== //// ==== //// ====






Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa