• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

Tarehe iliyowekwa: April 22nd, 2025

MKUU wa Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora, Mhe. Sauda Mtondoo amesema atachukua hatua dhidi ya hujuma ya kuweka uchafu, mchanga laini, maji au vikonyo katika zao la Pamba unaofanywa na baadhi ya watu.

 DC. Sauda ametoa ahadi hiyo Al hamisi mwezi Aprili 17, 2025, baada ya kutembelea Viwanda vya Manispaa ya Shinyanga akiwa na viongozi mbalimbali wa Chama cha Napinduzi (CCM) na Halmashauri.

Alisema msimu huu watahakikisha wanakua makini kuwasimamia viongozi wa AMCOS kwa lengo la kuhakikisha Pamba inakusanywa katika ubora unaotakiwa.

‘’Watu watakaojaribu kufanya uharibifu wa aina yoyote ni lazima tuchukue hatua stahiki na kali kwa lengo la kuhakikisha inakua fundisho kwa wengine wasijaribu kufanya hivyo kwa sababu ya kuendelea kulinda ubora wa Pamba inazalishwa Igunga,’’ alisema Mhe. DC. Sauda.

Aidha, aliahidi kukomesha uharibifu na uchafuzi unaodaiwa kufanywa na baadhi ya viongozi wa AMCOS katika maeneo ya ukusanyaji wa zao hilo.

Alieleza tabia hiyo isiyokua ya kiadilifu sio tu inazitia hasara Kampuni lakini pia serikali, hivyo nilazima wasimame kidete kwa kubanana kwa lengo la kuhakikisha msimu utakapoanza yasirudie yaliojitikeza katika msimu uliopita.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Igunga, Mafunda Temanya alisema wataendelea kutekeleza Ilani ya Chama ikiwemo kuwalinda wakulima wa Pamba.

 ‘’Ndani ya AMCOS kuna viongozi sio waaminifu ndio maana wanataka kuwachafua wakulima wakati wako vizuri, hivyo wanachafuliwa na Watu wajanja wajanja,’’ alisema.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Lucas Bugota alisema mpango wa kuzalisha Pamba umeipandisha Halmashauri hiyo kwa sababu inapata mapato ya kutosha, hivyo changamoto hiyo wameiona na kuahidi kuifanyia kazi kwa kuwasimamia wanaopokea Pamba.

Kwa Upande wa Mmiliki wa Kampuni ya Gaki Investment, Gasper Kileo alisema Mkulima anafikisha Pamba safi na inachafuliwa kwenye Ghala la kuhifadhia, hivyo aliomba Makatibu Meneja wapewe semina elekezi kwa sababu hakuna Mkulima anayekubali kuchafua mbegu au Pamba.

Alidokeza wanapata hasara ya moja kwa moja kwa sababu michanga inayokutwa kenye pamaba inaua mitambo ya uchakataji, hivyo wanaviomba Vyombo kuwa vikali dhidi ya watu wanaochanganya maji na mchanga kwenye Pamba.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Kampuni ya Fresho Investment, Salman Arab alisema msimu uliopita walipata hasara ya jumla sh. Milioni 650 zilizotokana na uchafu kwenye Pamba.

==== //// ==== //// ==== //// ====


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa