• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

MIPANGO YA IGUNGA KUWA KITALU CHA MBEGU YA PAMBA YAIVA.

Tarehe iliyowekwa: October 31st, 2023

 Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe. Sauda Mtondoo na wadau wengine wa Kilimo wamekutana kwenye kikao na kujadili mambo mbalimbali kubwa zaidi ikiwa ni kutangaza  kitalu cha uzalishaji mbegu za Pamba katika gazeti la serikali na Wadau wamekubali   kwa Kauli moja kwamba Igunga itangazwe rasmi kwenye gazeti la serikali kuwa  kitalu cha uzalishaji mbegu za pamba.

Katika hotuba yake Mgeni rasmi Mh.Sauda Mtondoo amewaomba viongozi wa upande wa chama na serikali kuwa na uelewa wa pamoja hasa viongozi ngazi ya kata  wote upande  wa chama na serikali kwa kuhakikisha   kwamba  kila mkulima wa zao la pamba anazingatia kanuni bora za kilimo cha pamba.

"Sisi viongozi wa serikali tushirikiane na viongozi wa Chama ili tuwe na uelewa wa pamoja maana sisi tukiwa na uelewa huo na wenzetu wa chama wasipokua na uelewa hatutafanikiwa", amesema Mhe. Mtondoo.

Ameongezea kuwa serikali inavyoendelea kuboresha zao hili na uzalishaji nao unazidi kukua na kwa mwaka huu uzalishaji umefikia Tani takribani 26,000 ambayo inaipatia mapato Halmashauri karibu bilioni moja.

Kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Igunga, kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kiserikali, wakulima na wadau wa kilimo sambamba na wadau kutoka Bodi ya Pamba Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi wake, James Shimbe.

Pamoja na mengi yaliyojadiliwa,  upatikanaji na uzalishaji wa mbegu katika kitalu cha pamba kilichopo Wilayani hapa ni jambo lililotiliwa mkazo huku ujumbe kutoka Bodi ya Pamba ukiahidi kutoa ushirikiano kikamilifu kuhakikisha zao hilo linazalishwa kisasa na kwa ubora.

Aidha kikao hicho kimeweka mpango mkakati wa kuwatafutia usafiri baadhi ya watendaji, ili kuwarahisishia namna ya kuwafikia kwa urahisi wakulima sambamba na kuendeleza kuwaelimisha, kusimamia na kukuza uzalishaji wa zao la pamba.

Vilevile,imeshauriwa si vyema zao la pamba kuchanganywa na mazao mengine kwani hupunguza ubora wa pamba.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa