Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga Bw; Athuman F. Msabila anautaarifu UMMA kuwa Halmashauri imepokea Fedha kutoka Serikali kuu kupitia Mradi wa SEQUIP Juni 2023 jumla ya Shilingi Billioni moja Millioni mia nne ishirini na saba na laki saba na Elfu themanini na moja na Shilingi mia moja ishirini na nne. (1,427,781,124). Fedha hizi ni kwa ajili ya kujenga Shule mpya mbili za Sekondari katika Vijiji vya Tambalale na Mtunguru,ujenzi huo wa Shule mpya umetengewa jumla ya shilingi 603,890,562.kila Shule.
Shule ya Tambalale ikikamilika itawapunguzia wanafunzi usumbufu wa kutembelea umbali mrefu kilomita 18 kutoka Tambalale hadi Simbo kila siku,pia wapo waliokuwa wanatembea kilomita 36 kila siku kwenda Shule ya Sekondari Simbo.Serikali ya awamu ya sita (6) inayoongozwa na Mhe; Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa mkombozi kwa Wananchi wa Igunga kwa kuwasogezea huduma za Elimu karibu yao.
Aidha Halmashauri imepokea Fedha shilingi (603,890,562) kwa ajili ya ujenzi Shule mpya ya Mtungulu. Fedha shilingi (110,000,000) kwa ajili ya ujenzi wa nyumba moja kwa mbili za walimu shule ya Sekondari Mwamakona,ambayo itakuwa na nafasi ya kutosha familia mbili za walimu.(two in one).
Shule ya Sekondari Seif Gulamali nayo imepata Fedha shilingi (110,000,000) kwa ajili ujenzi wa Nyumba moja kwa mbili (two in one) ya walimu,ambapo walimu wawili na familia zao wataishi katika nyumba hiyo na kuwarahisishia kazi yao ya kufundisha maana watakuwa karibu na maeneo ya kazi yao.
Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa