MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Mhe. Shabani Hemed amempongeza Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiletea Igunga fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo.
Aidha, ametoa zawadi kwa Mkuu wa shule ya sekondari Mwisi, Baraka Magoma na Mganga Mfawidhi kituo cha afya Ziba, Kassim Hashim huku Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari, Seleka Mtobi na Mkuu wa Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Lucia Kafumu wakipongezwa kwa kuwasimamia kikamilifu watumishi hao waliosimamia vema miradi ya maendeleo.
Mhe. Hemed ametoa pongezi na zawadi hizo leo, Ijuamaa Januari 30, 2026 wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani robo ya pili uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri mjini Igunga.
Amesema Dk. Samia ameleta hizi fedha kwa kutupendelea sisi wanaigunga ziwaletee wananchi maendeleo, hivyo amewataka wasimamizi kuwa na tabia ya kutembelea miradi na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara.
"Sisi sote ni viongozi na tunaowajibu wa kujua kila kitu kinachoendelea na kuwaeleza wananchi kwamba Dk. Samia Suluhu Hassan ameleta fedha zilizofanya kadha wa kadhaa," amesisitiza.
Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Sauda Mtondoo amesema serikali inafanya kazi kubwa ya kutafuta fedha na kuleta kutekeleza miradi mbalimbali, hivyo tuisimamie na kuhakikisha inakamilika kwa wakati na ubora.
Aidha, amewasisitiza kutunza mazingira kwa kupanda miti kwa lengo la kufikia malengo ya kupanda miti 1.5 milioni kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Pia, amewakumbusha viongozi hao kuwaelimisha wananchi kutumia vyoo na kufuata kanuni za afya kwa lengo la kuepukana na magonjwa ya mripuko.
Katika hatua nyingine, amewahimiza kuwakumbusha wazazi na walezi kuwapeleka watoto shule kwa lengo la kupata tija kupitia miundombinu mbalimbali iliyojengwa na serikali.
"Sisi viongozi tuliopewa dhamana tuwe mstari wa mbelee kutii maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na serikali na wananchi watafuata mlengo huo," amesema.
Akizungumza katika Mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Bi. Selwa Hamid amemshukuru Rais Dk. Samia kwa mema aliyowafanyia ikiwemo ushindi mkubwa alioupata katika uchaguzi Mkuu.
Amesema Halmashauri hiyo imepangiwa kukusanya sh. 6.9 bilioni, hivyo wanayo kazi kubwa kuhakikisha wanafikia asilimia 100 ya ukusanyaji.
Aidha, kwa upande wa miradi amesema wanamshukuru Rais Dk. Samia ambaye aliiletaa Halmashauri hiyo zaidi ya sh. 16 bilioni kutekeleza miundombinu mbalimbali katika majimbo ya wilaya hiyo.
============////////////////////////////////////


Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa