• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA, MHE. DEUS SANGU AMEMKABIDHI DHRO WA IGUNGA, HAMISI H. HAMISI TUZO YA USIMAMIZI BORA WA RASILIMALIWATU

Tarehe iliyowekwa: December 20th, 2024

NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu amemkabidhi Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Hamisi H. Hamisi Tuzo ya Usimamizi bora wa Rasilimaliwatu.

Mhe. Naibu Waziri amemkabidhi tuzo hiyo wakati wa Kikao cha Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma kilichofanyika katika Hoteli ya Halmashauri ya jiji la Dodoma jijini humo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Watumishi wa wilaya hiyo, wamempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Selwa Hamid ambae amekua akishirikiana vema na Mkuu wa Idara hiyo, Hamisi H. Hamisi kutoa huduma bora kwa watumishi, Madiwani na wananchi kwa ujumla.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Michezo na Utamaduni wa Halmashauri hiyo, Fadhil Kayange amesema ameipokea tuzo hiyo kwa furaha kwa sababu wameipata kutokana na hekima, busara na nidhamu ya kazi iliyopo kwa viongozi wao.

‘’Hakika viongozi wetu ni wasikivu wa changamoto zote zinazodaiwa kuwapata watumishi, binafsi ni mnufaika wa huduma bora wanazozitoa viongozi wetu ikiwemo kubadilishiwa muundo wa utumishi kutoka Mwalimu na kuwa Afisa Michezo Msaidizi, hivyo ninawapongeza na wanastahili tuzo hii,’’ amesema.

Kwa upande wa Afisa Mifugo Msaidizi Mkuu wa Halmashauri hiyo, Mohamed Kiswamba aliweka wazi kuwa wameipokea tuzo hiyo kwa furaha kwa sababu wanastahili kwa namna ambavyo wanachapa kazi kwa ushirikiano na ushirikishwaji kati yao na viongozi wao.

‘’Ninatoa wito kwa watumishi wenzangu wakiwemo viongozi wote tuendelee kuchapa kazi kwa kushirikiana kwa lengo la kueendelea kuonekana mfano wa kuigwa katika uongozi bora ikiwemo kukusanya mapato na kutoa huduma bora kwa wananchi,’’ amesema Kiswamba.

Naye Mwalimu wa Shule ya Msingi Mwanzugi, Yohana Uhwelo ameeleza kuwa  wameipokea tuzo hiyo kwa kishindo chenye uhalisia kwa sababu wamekuwa wakihudumiwa vizuri na Idara hiyo kutokana na ushirikano na uongozi bora, hivyo wanachapa kazi na wanaona ni haki yao.

Akiongea kwa njia ya Simu Mkuu wa Idara hiyo, Hamisi H. Hamisi amefafanua  kuwa  wamepata tuzo hiyo kwa sababu wamekuwa wakitekeleza vigezo vya Usimamizi wa Kanuni, Usimamizi mzuri wa Mifumo ya Kiutumishi, Usafi wa Mifumo, Utekelezaji wa Maagizo ya Viongozi na Usafishaji wa Taarifa za Watumishi.

Kufuatia tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Bi. Selwa Abdalla Hamid amesema ni jambo la kujivunia huku akiwapongeza watumishi wote na kuwataka kuendelea kuchapa kazi kwa weledi, maarifa, juhudi na busara kuwahudumia wananchi.
======/////=====/////=====/////=====


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa