• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

Waaswa Watendaji wa Vijiji Kufata Taratibu Kanuni na Sheria za Fedha

Tarehe iliyowekwa: March 18th, 2019

Mkagunzi wa hesabu za ndani Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Bwana Abdallah Habibu Mbuyu,mewataka  Watendaji wa Serikali za Vijiji kufata taratibu, Kanuni na Sheria na miongozo ya TASAF III katika zoezi la uhawailishaji fedha, alipokuwa katika zoezi la ukaguzi  namna zoezi linavyotekelezwa katika vijiji vya  Mwabubele, Kalangale, Buchenjegele, Mwamapuli, Chibiso na Mondo Wilayani Igunga.

“Nahitaji kujiridhisha kama fedha zinawafikia walegwa, kuhakikisha kama kuna ushiriki wa wajumbe wa serikali ya kijiji kwenye zoezi zima la uhawilishaji pamoja na wajumbe wa malipo CMC” ameongeza bwana Mbuyu makaguzi wa hesabu za ndani halmashauri ya Wilaya ya Igunga.

“Nasisitiza Serikali za vijiji kuweka utaratibu madhubuti wa fedha za walengwa zinazochukuliwa na ndugu wa mlengwa  mtoto, mjukuu, rafiki aiu mjumbe wa Serikali ya Kijiji na kuhakikisha fedha hiyo inamfikia mlengwa mwnyewe hata kama hajiwezi au ni mgonjwa ili kuondoa malamiko na manunguniko ya walengwa kukosa malipo yao” ameongenza Bwana Mbuyu mkaguzi wa hesabu za ndani halmashauri ya Wilaya ya Igunga.

“Nafatilia taratibu za uhawilishaji fedha pamoja na utunzaji wa kumbukumbu za malipo za kila siku za malipo na dirisha lililopita” ameongeza Bwana Mbuyu Mkaguzi wa Ndani Halmashauri ya Wilaya ya Igunga.

Bwana Abdallah Habibu Mbuyu akiongea na Kaimu Mtendaji wa Kijiji cha Mwabubele, Kalangale, Mwamapuli, Chibiso na Mondo amesisitiza wajumbe wa Serikali ya Kijiji kujiridhisha,kutembelea na kuangalia kama taratibu za malipo zinazingatiwa katika kila dirisha.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mondo na Chibiso wamesema kuna changamoto kubwa inayowakabiri ya ukosefu wa watendaji wa vijiji katika vijiji vyao, hali ambayo inasababisha utunzaji wa kumbukumbu za malipo kuwa ngumu, Kwani kukosekana kwa watendaji wa vijiji na  uongozi thabiti husababisha kutowewepo kwa kumbukumbu sahihi za malipo wanajitolea kukaimu hujiudhuru mara kwa mara.

Changamoto zinazojitokeza kwenye zoezi zima la uhawilishaji fedha moja ni kuchukuliana fedha kwa wale ambao hawajiwezi kufika eneo la malipo pamoja na wagonjwa.

Pia wajumba wa Serikali ya kijiji cha Mwabubele, Kalangale, Mwamapuli, Chibiso na Mondo wamesema kuna changamoto ya utoro kwa wanafunzi wanaotakiwa kutimiza masharti ya elimu kutokufika shule pamoja na wale wa masharti ya afya kutokupeleka watoto wao kliniki.

Nao walegwa wa TASAF III katika kijiji cha Chibiso na Mondo kata ya Choma wameeleza changamoto wanazokutana nazo pamoja na mafanikio  waliyoyapata amabayo ni pamoja na kupata chakula cha kutosha, kupeleka watoto shule na pamoja na kuweza kuchangia matibabu ya CHF.

“Nafuarahia kuwepo kwa Mradi huu wa TASAF III, kwani umeniwezesha kununua nguo na daftari za wanafunzi wanaosoma, Ng’ombe, viti vya kukalia nyumbani pamoja na kondoo watano” Bi, Panki Salawa ameongeza Mlengwa wa TASAF III kijiji cha Chibiso Kata ya Choma.

Bi.Dina Madeje Mratibu wa TASAF III Wilaya ya Igunga,amekiri kuwepo kwa changamoto ya watendaji wa vijiji walio wengi hasa vijiji vile ambavyo vimekaimiwa na wenyeviti wa vitongoji na baadhi ya wataalam katika zoezi la TASAF III, kumekuwa  na changamoto ya nyaraka nyingi kutopatikana kwa wakati na utunzaji wake kutokuwa mzuri kutokana na walio wengi kutokujua taratibu, kanuni na sharia  za fedha.

Imetolewa na

Kitengo cha TEHAMA na UHUSIANO

Halmashauri ya Wilaya ya Igunga.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa