• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

WANANCHI IGUNGA WAITIKIA KAMPENI YA MHE. RAIS DK. SAMIA MATUMIZI NISHATI SAFI

Tarehe iliyowekwa: February 12th, 2025

WANANCHI wa Wilaya ya Igunga mkoa wa Tabora wameunga mkono kivitendo kampeni ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi ya nishati safi baada kujitokeza kwa wingi kununua mitungi ya gesi na kuahidi kuachana na matumizi ya nishati chafu.

Akizungumza jana baada ya kununua nishati hiyo, Prisca Onesmo alisema wanaachana na matumizi ya kuni kwa sababu zimekua zinawaletea athari kwenye macho wanapokua wakipuliza moto wakati wa kupika.

Aidha, aliwashauri wanawake wanaotumia kuni waache kwa sababu serikali ya Rais Dk. Samia imetoa ruzuku kwenye nishati hiyo, hivyo mtu akiwa na namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) na sh. 20, 000 anapata mtungi wa gesi.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Nguvumoja wilayani hapa, Afred Nkuba alieleza kuwa Kampeni ambayo ameianzisha Rais Dk. Samia inawasaidia kwa sababu awali walikua wananua tela moja  la kuni kwa sh. 50,000 huku gunia la mkaa wakinunua kwa sh. 30,000, hivyo nishati ya gesi kuuzwa bei hiyo inawasaidia kuachana na matumizi ya nishati chafu ambayo licha ya kuwadhuru ni ghali kuipata.

‘’Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Dk. Samia kwa kampeni hii kwa sababu inawapunguzia wananchi kukata miti katika mapori yaliopo katika wilaya yetu,’’ alisema.

Naye Msimamizi wa Kampuni ya Gesi ya ORYX kanda ya Magharibi, Gibson Rodgers aliweka wazi kuwa wameisha uza majiko 13, 820 katika mkoa huo huku kwa upande wa wilaya ya Igunga wakiuza majiko 3255.

Pia, alieleza thamani halisi ya majiko hayo ni sh. 50, 000 lakini wameiuzia serikali kwa sh 40,000 ambapo Rais Dk. Samia emeweka ruzuku ya sh. 20,000 hivyo wanawauzia wananchi  nishati hiyo kwa sh. 20, 000 tu.

Kufuatia fursa hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Lucas Bugota aliwaomba wananchi waendelee kuunga mkono jitihada za Rais Dk. Samia na kumpa tena miaka mitano kwa sababu wanakinama wanajua kulea.

Akizungumza baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Halmashauri hiyo, Mkuu wa Wilaya hiyo, Sauda Mtondoo alisema Rais Dk. Samia anamaono makubwa ya namna ya kuwakomboa wananchi kuacha kutumia nishati chafu badala yake wajikite katika matumizi ya nishati safi.

Alieleza kuwa Dk. Samia amekua mtu wa mbele (Champion) na kushika nafasi ya pili barani Afrika, hivyo wanakila sababu ya kuhakikisha wanamfanya awe namba moja Afrika.

Aliwahimiza wananchi kuelekeza nguvu zao katika matumizi ya nishati safi kwa sababu wanaamini itakuwa ni suluhisho la kutunza mazingira na kuwaokoa akinamama na maradhi yanayotokana na matumizi ya nishati chafu.

==== //// ==== //// ==== //// ====


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa