• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

WANANCHI WAMETAKIWA KUTUMIA KURASA RASMI ZA MITANDAO YA KIJAMII YA SERIKALI KUJUA FURSA ZILIZOPO IKIWEMO MIKOPO MBALIMBALI

Tarehe iliyowekwa: January 11th, 2025

WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhe. Dk. Dorothy Gwajima ameitaka jamii kubadili mtazamo wanapopita katika kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii na kufuatilia kurasa za mitando ya serikali kwa lengo la kuelewa namna ambavyo Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan alivyoleta maendelo kwa jamii na Mtu mmoja mmoja.

Mhe. Waziri Dorothy ameyasema hayo Ijumaa Januari 10, 2025 wakati akizindua kikundi  cha Wanawake  kijiji cha Mwanzugi kilichopewa sh milioni 30 na Halmashauri ya wilaya ya Igunga mkoani Tabora.

Alisema wanapoyapokea hayo maendeleo na kuyatafsiri wasikatishwe tamaa wayataje kwa lengo la kuhakikisha wale wasio kubali kwenda na serikali inapotaka kwenda au watafute njia yao waende wanakotaka kwenda wayaone.

Alieleza kuwa serikali inafikika na ipo kiganjani kwao kidijitali hivyo wasikubali kufangamana na watu wanaowakatisha tamaa kupata stahìki zao za msingi ikiwemo mikopo inayotolewa na serikali.

"Maendeleo wanaweza kuletewa wayasikilize au wayatafute wayaone mfano tangu Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan aingie madarakani mkoa wa Tabora uliishapokea zaidi ya sh Trilioni 1.1 kusukuma na kuleta maendeleo ya  miradi katika sekta zote " alisema.

Aidha, alisema ni jukumu lao kuyataja maendeleo, kutafuta taarifa zake wanazozitoa kila siku kwa lengo la kupata maneno ambayo watayazungumza kwa watu wanaodaiwa kutotaka kukubali kwamba Mhe. Rais Dk. Samia amefanya maendeleo wasikie na wayaone.

" Ndugu wananchi ! Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan anajenga miundombinu ya uchumi mifukoni mwa vikundi na mtu mmoja mmoja ikiwemo Wanaume kupitia Baraza la Uwekezaji Wananchi Kiuchumi kuna mifuko zaidi ya 100," alisema.

Alidokeza kuwa  mwaka 2024, Rais Dk. Samia alianzisha programu inayowagusa sio wanawake tu wakiwemo wanaume wanaofanya biashara ndogondogo.

Aliweka wazi kuwa mkopo huo ulipitishwa na Bunge takribani sh. bilioni 10.5  huku sh. bilioni tano tayari zimeishatolewa kwa lengo la kuona kasi ya kuzikopa kutoka kwenye benki ya NMB ambayo ilishinda zabuni.

Kutokana na hayo, aliwahimiza watafute habari kwenye kurasa rasmi za serikali za mitandao ya  kijamii ikiwemo kusikiliza radio na kutazama televisheni kwa kuwa serikali imeendelea kuzindua mikopo mbalimbali ya kuwawezesha Watanzania kiuchumi.

Alibainisha kuwa kunamkopo mwingine wameuzindua mwezi Disemba,2024 kwa lengo la kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dk. Samia kwamba pamoja na mkopo wa asilimia 10 unaotolewa kwenye Halmashauri inchini wazindue mwingine unaoitwa Pamoja Programu utakaoongeza uwezashaji wa Wanawake kiuchumi.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Igunga, Athuman Mdoe alimpongeza Mhe. Rais Dk. Samia kwa kuendelea kuinufaisha kata hiyo kwa sababu walipata fedha sh. milioni 603 kujenga shule ya sekondari, milioni 561 shule ya msingi na watoto wanasomea huku sh. milioni 361 zimekamilisha madarasa shule ya sekondari Mwanzugi.

Naye Mwenyekiti wa kikundi cha Mwendo kasi, Telezia Nkamba aliwataka Wanawake kuchangamkia fursa na kuacha tabia ya kukaa kwa sababu sasa hivi sio zama za kanga, vitenge na kuendesha majungu.

"Hatuwezi kufanikiwa tukiwa na majungu ya pembeni , njooni mjifunze tuwasadie la kufanya kwa sisi tuliopiga hatua tuendelee kutafuta maisha na kuisaidia jamii na watoto wetu" alisisitiza.
====== ////// ==== ////// ======





Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa