• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

WANAWAKE IGUNGA WAWASHIKA MKONO WAGONJWA KUELEKEA KILELE SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE

Tarehe iliyowekwa: March 7th, 2025

UMOJA wa Wanawake wa Wilaya ya Igunga mkoa wa Tabora wamefanya zaira ya kuwatembelea na kuwashika mkono wagonjwa mbalimbali waliopo katika Hospitali ya Wilaya hiyo ikiwa ni sehemu ya kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Wanawake.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Afisa Tarafa wa Kata ya Igunga, Advella Kakuru aliwashukuru Wanawake hao kwa namna ambavyo wamejitoa kwa lengo la kuhakikisha wenzao waliokua katika halimbalimbali wanakuwa na furaha mfano wa waliyonayo wao.

‘’Leo tukiwa tunaelekea kuadhimisha siku ya mwanamke duniani umoja wetu umeona uwashike mkono kwa sababu sisi sote ni akinamama, hivyo tunaelewa ilivyo kazi kulea na kuuguza,’’ alisema na Kuongeza kuwa:

‘’Chochote ambacho mmechanga na mmetoa kwa wenzetu hawa tunamuomba Mwenyezi Mungu awalipe badala, hivyo tuendelee na umoja huu kwa lengo la kuhakikisha mwakani tunayafikia makundi mengine wakiwemo watoto yatima na wafungwa.’’

Aidha, aliwaomba wagonjwa kuendelea kuwa na faraja kwa sababu wanawake wote waliowatembelea wanawatia moyo na wanaamini Mwenyezi Mungu atawafanyia wepesi na watapona maradhi yanayowasibu.

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Grace Nyamwanji alisema wameungana na Wanawake walipo Wodini ambao wanauguza kuwashika mkono kwa baadhi ya mahitaji kwa lengo la kuwaweka karibu wasijisikie upweke.

‘’Tunaomba mfahamu sisi tuko pamoja na nyinyi kwa sababu sisi sote ni walezi na tuliishawahi kuuguza, hivyo jisikieni faraja tuko pamoja,’’ alisema.

Akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Afisa Afya, John Masesa aliwapongeza Wanawake hao kwa sababu matendo ya huruma waliyoyafanya ni makubwa na niibada.

Aidha, alisema kazi ya Mama katika jamii ni kubwa kwa sababu kama si akinamama wasingekuwepo, hivyo waendelee kuwaombea akinababa kwa lengo la kuhakikisha Wanakaa sawa.

‘’Ninashukuru sana na kuwaomba muendelee kutulea na kututunza kwa sababu ni moja ya wajibu wenu na tuombe jamii iendelee kuwa na afya njema itekeleze majukumu yake,’’ alisema.

Kwa Upande wa Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Scholastica Ikandilo alieleza kuwa wanajitahidi katika kutoa huduma bora, hivyo kuna mabadiliko makubwa kwa sababu Wauguzi walionao wanatekeleza maadili ya kazi zao.

‘’Nitoe wito kwa jamii wanapokua na ushauri wasisite kutueleza na sisi tutaufanyia kazi kwa sababu sisi tulipata elimu hizi kwa lengo la kuhudumia jamii na sio kukaa na elimu zetu nyumbani,’’ alitoa wito.

Naye mmoja wa Wazazi, Hadija Shabani aliwashukuru Wanawake hao kwa kuwajali na kuwathamni huku akiwaomba wasisite kuendelea na moyo huo.

‘’Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwaongoza kuja kututembelea wanawake wenzenu ninamuomba Mungu awabariki na kuwaongezea kwa kile mlichotoa,’’ alishukuru.

Umoja wa wanawake huo, umemtembelea Hadija Shabani mama wa Mapacha walikua wameungana na kutenganishwa ambao kwa sasa wanaishi Nkokoto Igunga na kuwatembelea wagonjwa Wodi ya Watoto chini ya miaka mitano, Wodi ya watoto wagonjwa na waliolazwa na uzito pungufu (NICU) , Wodi ya Wazazi wanaotarajia kujifungua , waliojifungua na ICU.

==== //// ==== //// ==== //// ====


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa