• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

Tarehe iliyowekwa: March 9th, 2025

KAIMU Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Mhe. Dk. Khamis Mkanachi amesema Wanawake ni kundi kubwa katika jamii linaloongoza  kwa wingi sio tu Tanzania  mpaka duniani.


Dk. Mkanachi ameyasema hayo leo Jumamosi Machi 8, 2025  wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake yaliofanyika Kimkoa katika uwanja wa Samora Nzega Mji.


Alisema mazingira nchini ni rafiki, hivyo Wanawake wenyewe waendelee kuangalia namna  wanawezaje kupata haki na usawa wanaoutaka ikiwemo kukabiliana na mambo ya kiuchumi.


"" Ndugu zangu ninamnukuu Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa Wanawake sio dhaifu, wanawake ni Mahiri, shupavu na wananguvu ," alinukuu.


Aidha katika kuwawezesha kiuchumi, alisema mkoa huo umewawezesha Wanawake hao mikopo ya asilimia 10  kutoka mwezi Januari mwaka 2024 hadi mwezi Machi 2025 sh. Bilioni 3.9.


Alifafanua kuwa Vikundi vya Wanawake  226 vilipata takriban sh. bilioni 1.9, vijana vikundi 127  walipata sh. bilioni 1.7 huku walemavu vikundi 32 wakipata sh. milioni 265.5.


Katika hatua nyingine, Dk. Mkanachi aliweka wazi kuwa Mwanamke ndio  mwalimu wakwanza wa kiumbe yoyote anayekuja duniani.


"Mwanamke ni kama mwalimu, anasimama kama afisa mipango nyumbani, mchumi mwenye kujua bajeti ndogo na kubwa ya uwekezaji, mratibu wa mambo yote ya kifamilia na ni afisa uhusiano anayejenga na kuwaunganisha kati ya ndugu na watu wengine, familia na ukoo ikiwemo lugha nzuri ambayo ni tiba ndani ya familia," alisema.


Hata hivyo, aliwakumbusha wazazi pamoja na kutafuta fedha wasisahau malezi ikiwemo kuwasikiliza watoto na kuwalinda dhidi ya mmomonyoko wa maadili.


Akizungumzia kuhusu uchaguzi, aliwashajiisha wajitokeze kugombea na kupiga kura kwa wingi wakiamini kwa wingi wao watapata ushindi wa kishindo.


"Niwaombe wanawake wote tumuahidi Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ushindi wa kishindo kwa sababu kura zake sio za mashaka kwa idadi ya wingi wa wanawake," aliahidi.

Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake huadhimishwa kila ifikapo  tarehe 8  Mwezi Machi ya kila mwaka.

==== //// ==== //// ==== //// ====


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa