• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI WASISITIZWA KUTUMIA MIFUMO KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO

Tarehe iliyowekwa: February 5th, 2025

MAENDELEO ya Sayansi na Teknolojia yanayoendelea kutekelezwa nchini hususan katika kutumia mifumo mbalimbali kutekeleza majukumu yamewaibua Watendaji wa Kata na Vijiji wa Wilaya ya Igunga mkoani Tabora kuiomba Serikali kuwatazama watumishi hao.

Wakizungumza katika kikao Kazi jana, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo chenye lengo la kijifundisha mfumo wa FFARS, Watumishi hao wameomba kupatiwa nyenzo za kisasa ikiwemo vishikwambi kwa lengo la kukabiliana na mabadiliko hayo.

Mtendaji wa Kijiji cha Mwaomba kata ya Igurubi wa wilaya hiyo, Baraka Julias alisema wanaiomba serikali kupitia Wizara ya TAMISEMI iwakumbeke Watendaji wa Kata na Vijiji kuwapatia vifaa vitakavyowawezesha kupata mifumo waliyofundishwa.

Kwa upande wa Mtendaji wa kijiji cha Mwakabuta, Revocatus Shamba aliishukuru Idara ya Fedha kwa kuendesha mafunzo hayo na kuomba Watendaji wa Vijiji na Kata wawezeshwe kupata Vishikwambi.

‘’Mafunzo haya yamenijengea uwezo, nimetambua dunia imehama kutoka analoji kuwa dijitali, hivyo ninaomba Watendaji wa Vijiji tuwezeshwe Vishikwambi,’’ aliomba.

Mtendaji wa Kata ya Ziba wilayani hapa, Daniel Jinge aliomba kuhusu mifumpo inayoongezeka ni vema wakaendelea kupewa mafunzo kwa lengo la kuendelea kuongeza ufanisi katika majukumu yao.

Kutokana na maombi hayo, Mkuu wa Kitengo cha Fedha wilayani hapa, Mpakani Kalinga aliweka wazi namna ambavyo Utawala umejipanga kuitatua changamoto hiyo ya kutokua na Vishikwambi kwa kipindi hichi kwa kuanzisha chumba maalumu ambacho Watendaji watakitumia kufanya maandalizi ya malipo, kusainisha kisha kwenda benki.

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Wilaya hiyo, Hamisi Hamisi aliwataka Watendaji wanaodaiwa kuwa na tabia ya ulevi, uvivu na majibu mabaya kwa wananchi kuacha tabia hiyo.

‘’Serikali inawajali watumishi, hivyo kwa nini mshindwe kuwahudumia Wananchi vizuri, mliomba kazi kafanyeni kazi, hivyo sipo tayari kusikia migogoro ambayo ilitakiwa itatuliwe katika ngazi zenu inaletwa Halmashauri,’’ alisisitiiza.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Grace Nyamwanji aliwataka Watendaji hao kwenda kufanya usuluhishi wa fedha zilizoko benki kwa kulinganisha taarifa zilizopo katika vitabu vyao na kuziwasilisha kabla ya tarehe 7 mwezi huu.

‘’Ninawasisitiza ndugu viongozi mmepewa mafunzo haya mwende mkatekeleze hili kwa wakati,’’ alihimiza.

Mafunzo ya Mfumo wa FFARS kwa Watendaji wa Kata 35 na Vijiji 119 yalihusisha mada ya Mapokezi ya Fedha, Usuluhishi wa Kibenki, Kufanya Usuluhishi katika Mfumo na Maelezo kuhusu Mfumo wa Nest.

==== //// ==== //// ====


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa