• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

WATUMISHI WA AFA IGUNGA WAMEPONGEZWA KUDUMISHA UADILIFU NA KUTOA HUDUMA RAFIKI KAZINI

Tarehe iliyowekwa: January 18th, 2025

WAFAWIDHI wilayani Igunga mkoani Tabora wamekutana katika kikao kazi Alhamisi Jaunuari 16, 2025 katika ukumbi wa St. Leo kujadili Bajeti, Matumizi ya Fedha, Bima ya Afya ya Taifa (NHIF), Taarifa ya Mapato robo ya kwanza na ya pili mwaka 2024 hadi 2025 ikiwemo maelekezo ya namna ya kupokea fedha kwenye mfumo na kufanya usuluhisho wa fedha zilizoko benki na matumizi.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Bi. Selwa Abdalla Hamid ambae alikua mgeni rasmi katika kikao hicho alianza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoendelea kuijali Halmashauri hiyo kwa kuipatia fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo.



‘’Ninamshukuru Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutuwezesha kwenye rasilimaliwatu, kiuchumi, miundombinu na kupata fedha sh. milioni 100 za kuwakopesha Wajasiriamali wadogowadogo,’’ alishukuru.


Pia,  aliwapongeza Waganga Wafawidhi na Watumishi wote wa Afya kwa namna wanavyotoa huduma za afya vizuri kwa wananchi, hivyo kuwahakikisha kwamba kadri wanavyoendelea kutimiza wajibu wao ndivyo utawala utakavyoendelea kuwajali.



Aliwahimiza kuhakikisha wanapeleka fedha zitokanazo na mapato kutoka kwenye vituo vyao benki na kuhakikisha zinasoma kwenye mfumo kisha waziombe kwa kufuata muongozo uliopo kwa lengo la kuendelea kufanya matumizi.


‘’Asiruhusiwe mtu yoyote kuchukua fedha ambayo haijaingizwa kwenye mfumo na kupelekwa benki,’’ aliagiza.


Pia, aliwakumbusha kuendelea  kufanya usuluhisho wa kifedha kati ya zile zilizopo benki na matumizi kwa wakati kwa sababu tabia hii itawaondolea mzigo, hivyo wataweza kutekeleza shughuli zao kirahisi.


Aliwataka kuhakikisha wanaendelea kuwasimamia watumishi waliopo katika vituo vyao kwa lengo la kuendelea kufanya vizuri katika usimamizi wa rasilimali watu.


‘’Mmepewa majukumu simamieni na ikitokea kuna mtumishi amekiuka taratibu au anawaharibia kazi mwambieni na msimuonee aibu kwa sababu msipo chukua hatua atawaharibia kazi,’’ alishauri.


Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Lucia Kafumu aliwakumbusha Wataalamu hao kuwa wamefanya kikao kazi hicho mwezi Januari kwa lengo la kupeana mwelekeo wa namna ya kuendelea kutoa huduma vema na waweze kutembea pamoja.


Kwa upande wa Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Halmashauri hiyo, Hamisi Hamisi aliwahimiza Watumishi hao kuendelea kuwa waaminifu, kuepuka rushwa, kuepuka unyanyasaji wa kijinsia, kuziishi kanuni za utumishi wa umma na kuwa na matumizi sahihi ya madaraka.


‘’Ndugu Watumishi wenzangu niwaombe tuendelee kujichunga na vitu vinavyoaibisha Utumishi wa Umma ikiwemo ulevi, kamari, kugombana na kubeti,’’ alionya.


Naye Afisa Tabibu wa Zahanati ya Mwanyagula, Ramadhan Murad aliahidi kuyafanyia kazi mambo yote yaliozungumzwa katika kikao hicho ikiwemo kuendelea kutoa huduma rafiki kwa wananchi.


‘’Tukuahidi Mkurugenzi wetu tutakusanya vizuri mapato, tutabenki na kufanya usuluhishi wa kifedha kati ya matumizi na fedha zilizopo benki kwa wakati,’’ aliahidi.

==== //// ==== //// ==== //// ====



Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa