• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

WATUMISHI WAASWA KUTEKELEZA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

Tarehe iliyowekwa: August 22nd, 2018

 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa (MB), amewaasa watumishi wa Serikali kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi akiongea nao katika kikao cha kazi cha kufatilia shughulia za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga hivi karibuni.

 

“unaweza ukawa ni mpenzi wa chama kingine hauzuiliwi, lakini ni muhimu ujue kwamba ndani yako unatekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi ndiyo chama kinachounda Serikali,na maagizo unayofanya wewe kama mtumishi wa Serikali yanatokana na ilani ya Chama cha Mapinduzi huna sababu yakuonyesha shida ya kutekeleza wajibu wako” alisema Mheshimiwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Ziara hizi zinamadhumuni ya kufahamiana,kukumbushana wajibu na vile vile kuwapa msimamo wa Serikali kujihakikishia kama mambo yanakwenda vizuri” aliongeza kusema Mheshimiwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Jukumu lenu ni kuhakikisha mnawatumikia wananchi wa Igunga, mpo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi, wananchi hawatakiwi kulalamika na watumishi mkiwepo katika maeneo haya, Serikali inawaamini watumishi ni wasomi,hivyo ni muhimu kujihakikishia shughuli  za kila siku zinaleta mafanikio kwa wananchi wala siyo mafanikio tu na mwananchi anatarajia kuona uwepo wako unatija na lazima uwepo mpango wa kazi wa kila siku, wa robo mwaka, nusu mwaka na mwaka mzima.

Alisisitiza watumishi kutumia muda wao kuwatembelea wananchi kujua shughuli zinavyoendelea katika sekta zote za Elimu, Afya, maji,Kilimo na upande wa barabara.Wananchi wanahitaji kujua Halmashauri yao ina mpango gani juu ya Kata na vijiji vyao. Pia aliwaambia shughuli za mikutano ya hadhara si ya wanasiasa tu, bali hata wakuu wa idara wanawajibu wa kufanya mikutano, ili kuwaelimisheni wananchi kujua mipango ya halmashauri yao na serikali yao.Hivyo katibu tawala wa wilaya ni wajibu wake kuwasimamia watumishi ndani ya wilaya, na ndiye mkuu wa watumishi ndani ya wilaya.

Kwa Sekta ya Afya ameagiza kila kijiji kuwa na zahanati, kila kijiji kijenge zahanati yao na Daktari wa Wilaya (DMO) na timu yake ya wataalam ifanye mikakati kupitia mwenyekiti wa halmashauri kwenye mipango ya halmashauri kuhakikisha inasaidia vijiji kwa kuwapatia simenti na bati. Serikali imedhamiria kuona kuanzia ngazi ya kijiji kuna Zahanati.

Kwenye Elimu kunahiatajika kusimamiwa kikamilifu. Mkoa wa Tabora  uko nyuma kielimu, maafisa elimu mpo, wasomaji wapo walimu wapo japo hawatoshi, haya yote yanatokana na utoro unaosababishwa na wazazi kupeleka watoto kuchunga mifugo na mimba za utotoni.  Ni jukumu la sekta ya Elimu kusimamia na kuyakemea  haya kwani yanasababisha elimu kushuka.

 Katika Mkutano wa hadhara viwanja vya manadani Igunga Mhe. Waziri Mkuu alisema ”Utumishi wanaotakiwa kutoa siyo ule wenye dalidali za usumbufu kwa wananchi nimekemea tabia ya njoo kesho njoo kesho njoo kesho maofisini tunaamini wale ni wasomi wamesoma vizuri kwenye maeneo yao waliyoajiliwa” aliongeza Mhe.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Mheshimiwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (MB), ameendelea kuwakumbusha watumishi kujituma na kusimamia kazi zao kwani wameletwa kwa makusudi katika eneo hili la Igunga, kuwatumikia wananchi na  wamebobea kwenye taaaluma zao.Na watumie muda wao kuwatembelea wananchi vijijini kufatilia maendeleo ya miradi inayoletwa na serikali.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa