• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

Idara ya Elimu Msingi

Idara ya Elimu Msingi Katika Halmashauri ya wilaya ya Igunga ni moja ya idara ambayo inatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Mtaala wa Elimu ya msingi na mtaala wa Elimu ya awali ambayo imeandaliwa kwa kuzingatia viwango vinavyokidhi haja ya kujifunza kwa ufanisi ili kumjengea mwanafunzi umahiri wa elimu ya awali na msingi kwa kuzingatia matakwa ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014. Sera hiyo inaelekeza kuwa elimu msingi ni ya lazima kwa kila mtoto wa Tanzania.

Sekta ya elimu na mafunzo, kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo  ya Taifa ya 2025 na mpango wa muda mrefu wa maendeleo ya Taifa 2011/12 hadi 2014/25, inatarajiwa kuleta maendeleo ya haraka ya rasilimali watu kwa kutayarisha idadi ya kutosha ya Watanzania walioelimika na kupenda kujielimisha zaidi ili kulifanya Taifa lipate maendeleo na kuwa lenye uchumi wa kati na shindani ifikapo 2025.

Katika Wilaya ya Igunga huduma ya utoaji elimu ya Awali na  Msingi inafanyika kwa ushirikiano kati ya Halmashauri na wadau mbalimbali wa maendeleo waliopo katika Wilaya. Halmashauri ina jumla ya shule za Msingi 137 zilizosajiliwa, ambapo Shule 133 ziko chini ya umiliki wa serikali 1 zinamilikiwa na watu binafsi na 3 zinamilikiwa na taasisi za dini. Aidha usimamizi wa shule uko chini ya afisa Elimu Msingi katika ngazi ya Wilaya na Afisa Elimu Kata kwa ngazi ya kata.

Idara ya Elimu Msingi inaundwa na vitengo vitatu katika kutekeleza majukumu yake. Vitengo hivi ni kama ifuatavyo:-

  • Elimu ya watu wazima
  • Taaluma
  • Takwimu
  • Utamaduni na michezo

 MAJUKUMU YA IDARA YA ELIMU MSINGI 

  1. Kupanga, kuratibu na kusimamia wajibu na maslahi ya watumishi katika Idara ya Elimu ndani ya Wilaya
  2. Kupanua na kuimarisha Elimu ya,Awali, Msingi na Elimu ya watu wazima katika Wilaya
  3. Kukagua na kufuatilia taarifa za ukaguzi wa Elimu ya Msingi na kutoa ushauri kwa walimu juu ya utekelezaji wa mitaala ya elimu
  4. Kuandaa na kusimamia uendeshaji wa mitihani ya Elimu ya Msingi hasa darasa la IV na VII ya Taifa kila mwaka.
  5. Kusimamia mgawo na mipango ya fedha kwa ajili ya uendeshaji masuala ya kielimu
  6. Kuwaendeleza walimu kitaaluma ili watoe huduma bora zinazokidhi viwango
  7. Kukusanya takwimu za watahiniwa wa darasa la IV na VII kutoka shuleni kuzihakiki na kuziwasilisha Mkoani kila mwaka
  8. Kuagiza na kusambaza vifaa vya elimu katika shule, kugawa fedha na kusimamia matumizi ya fedha katika shule
  9. Kubaini na kusimamia ikama ya walimu katika shule, kusimamia na kufuatilia miradi ya ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu, vyoo na utengenezaji samani za shule
  10. Kusimamia uanzishaji na uendeshaji wa maktaba za Kata na Vijiji
  11. Kushirikiana na sekta za Afya, M/jamii na mashirika ya Umma kuendeleza Elimu Maalum kwa shule za Msingi
  12. Kupanga, kuratibu na kusimamia michezo, kusimamia sera za michezo na utamaduni wa Kitanzania katika shule za msingi

Matangazo

  • TANGAZO LA KUAHIRISHWA KWA USAILI July 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI MAALUMU YA KUKUSANYA USHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA IGUNGA August 24, 2021
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA September 27, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • UGAWAJI WA PIKIPIKI KWA WATENDAJI WA KATA 9

    July 18, 2022
  • Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Igunga Bi Fatuma O. Latu

    March 08, 2022
  • Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Igunga Bi Fatuma O. Latu

    March 05, 2022
  • Mhe Mkuu wa wilaya ya Igunga Bi Sauda Mtondoo amekabidhi madawati kwa shule za Sekondari yaliotengenezwa kwa fedha za mapato ya Ndani ili kukabiliana na upungufu wa madawati shuleni.

    March 05, 2022
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa