• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

Uvuvi na Mifugo

Idara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi katika Halmashauri ya wilaya ya Igunga, ilikuwa sehemu ya Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika.  Iliundwa rasmi mwaka 2012/2013, kutokana na agizo la serikali la kutaka iwe Idara inayojitegemea ili kuongeza uwajibikaji na ufanisi kwa sekta hii muhimu. Lengo kuu la Idara hii ni kusimamia na kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi, ili ziwe zenye tija, ufanisi na ushindani, zinazochangia kuboresha hali za wananchi  wa wilaya ya Igunga ambao ufugaji na uvuvi ni sehemu ya shughuli zao za kila siku na zenye kuzingatia hifadhi ya mazingira. Malengo mahsusi ya Idara, ni pamoja na kuboresha koosafu za mifugo ya asili, kuboresha malisho ya asili na kudhibiti matumizi bora ya ardhi, kuzuia na kudhibiti magonjwa ya mifugo na kuboresha masoko ya mifugo na mazao yake. Majukumu ya idara ni pamoja na kuratibu, kusimamia, kufuatilia, kutekeleza  Sera, Sheria, Kanuni, Miongozo na Maagizo yanayohusu shughuli zote za maendeleo ya sekta za mifugo na uvuvi, kwa  kushiriki na kushirikisha wadau wote wa maendeleo na hifadhi ya mazingira.

Idara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi inaundwa na sehemu mbili, yaani mifugo na uvuvi, zenye wataalam wa fani mbalimbali, zikiwemo, udaktari wa wanyama, sayansi ya uzalishaji wanyama, sayansi ya uzalishaji, utumiaji, hifadhi na uendelezaji wa nyanda za malisho, wataalam wa wanyama wadogo, kuku, masoko ya mifugo na mazao yake, tiba na afya ya mifugo, uhimilishaji, uanzishaji na uendeshaji wa mashamba darasa ya mifugo, usimamizi na ufuatiliaji wa program za ugani. Idara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ina jumla ya watumishi 34, ambapo watumishi 9 wapo makao makuu ya wilaya na wengine 25 wapo ngazi ya kata. Shughuli wanazofanya wataalam hawa ni pamoja na kutoa ushauri wa ufugaji bora wa mifugo na samaki, kuwezesha uundaji wa vikundi  na vyama vya wafugaji, kuratibu, kusimamia na kufuatilia  afya ya mifugo, kinga na matibabu ya mifugo, ukaguzi wa nyama na usafi wa machinjio, kukusanya maduhuli ya serikali, kuratibu, kusimamia na kufuatilia masoko ya mifugo na samaki, kukusanya takwimu za mifugo na mazao yake  na kusimamia utekelezaji wa sera, sheria, kanuni, miongozo na maagizo yanayohusu maendeleo ya sekta za mifugo na uvuvi wilayani.

Majukumu ya Idara ya Mifugo na Uvuvi

  1. Kusimamia maendeleo ya sekta ya mifugo na uvuvi.
  2. Kuratibu uundaji na uendeshaji wa vikundi na vyama vya wafugaji.
  3. Kuratibu, kufuatilia, kusimamia, nakutathimini utekelezaji wa sheria, kanuni, miongozo, na maagizo yahusuyo sekta ya mifugo na uvuvi.
  4. Kuandaa taarifa za utekelezaji wa shughuli za mifugo na uvuvi za mwezi , robo, nusu na mwaka.
  5. Kuandaa taarifa za utekelezaji za watumishi wa sekta ya mifugo na uvuvi.
  6. Kutathimini mahitaji, upatikanaji na usambazaji wa pembejeo na zana za mifugo.
  7. Kusimamia ukusanyaji wa maduhuli ya serikali yahusuyo sekta ya mifugo na uvuvi.
  8. Kuratibu na kusimamia utambuzi usajili na matumizi ya nyanda za malisho na upatikanaji wa vyakula vya mifugo na samaki.
  9. Kuratibu na kusimamia kuzuia na udhibiti magonjwa ya mifugo na samaki.
  10. Kuratibu na kusimamia programu za elimu kwa umma juu ya sekta ya mifugo na uvuvi.
  11. Kubuni na kutoa ushauri wa sera za mikakati ya kuendeleza na kudumisha afya za mifugo na uvuvi.
  12. Kuratibu kusimamia na kufuatilia mfumo wa miundombinu masoko ya mifugo na mazao yake pamoja na viwango wa ubora.
  13. Kuendeleza na kuimarisha uhusiano wa kisekta kati ya dara za halmashauri.
  14. Kuandaa na kutekeleza bajeti ya maendeleo ya mifugo na uvuvi.

 

Nb: Wataalam waliopo wilayani ni Dr. Emmanuel Masaki (BVM -VO I) – Afisa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi (W);Mr. Andreas Kafuru (BSc. An. Sc. AHD, AHPC -SLO) – Afisa Mifugo (W); Mr. Steven Mdaki (MSc. Agr. Ext. Educ, BSc. Range Mngt, AHD.-LO I) SMS (Uendelezaji nyanda za malisho);Mr. Paul Mtani (Dip. Range Mngt.-PLFO I) – Afisa Masoko ya mifugo; Ms Martha Rwiza (Dip. Poultry Prod.-PLFO I) SMS (Uzalishaji kuku na wanyama wadogo wadogo);Mr. Mohamed Kiswamba (AHD-LFO I) SMS(Afya ya Mifugo na udhibiti magonjwa ya mifugo): Mr. David Sengo (AHD-PLFO I) Focal person (Ngozi): Mr. Ezra Lema (AHD-PLFO I) – Afisa Ugani (W): Mr. Lazari Mushi (Dip. Range Mngt.-PLFO I) Kaimu Afisa Uvuvi (W).

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa