MKUU wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Ndug. Hamisi H. Hamisi amempongeza Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha maslahi ya Watumishi ikiwemo fedha za likizo.
Ndug. Hamisi ametoa pongezi hizo, Jumatatu Februari 02, 2026 wakati wa kikao kazi na Watumishi wa kata ya Igunga, Bukoko na Mtungulu kilichofanyika katika ukumbi wa Father Albert Bolle mjini hapa.
"Ni fahari kwetu watumishi kwa sababu Mhe. Rais. Dk. Samia Suluhu Hassan katuletea fedha za likizo za kutosha na katuongezea mishahara ikiwemo kupandisha vyeo," amesema.
Aidha, amewataka Watumishi hao, kuendelea kufanya kazi kwa weledi na wasione tabu kwa sababu waliomba kazi na wamepata kazi hivyo wasione kazi kufanya kazi.
Pia, amewahimiza kuhakikisha wanafuata maadili ya utumishi wa umma ikiwemo nidhamu yakutekeleza majukumu yao katika vituo vyao vya kazi.
"Niwaombe watumishi wenzangu kutii mamlaka na kutekeleza yale yanayoagizwa na viongozi wetu kwa sababu kutofanya hivyo ni makosa yanayosababisha kumchukulia hatua za kinidhamu mtumishi," amesema.
Amewataka kutumia mishahara wanayoipata vema na isewe sababu yakuwafukuzisha kazi kwa kuwa walevi, kukopa kunakomfanya mtumishi kutokwenda kazini na kugawa kadi kwenye taasisi za mikopo.
Katika hatua nyingine, amewakumbusha watumishi hao kuwa walezi wa wanafunzi nakutojiuhusisha na vitendo vya ngono nao kwa sababu kufanya hivyo ni kinyume na sheria za utumishi na nchi.
"Nivizuri kila mtumishi kuhakikisha anafuata maadili, anatoa huduma bora, anaitii serikali, anatoa huduma bila upendeleo, anawajibika kwa umma na anaheshimu sheria za utumishi wa umma, " amesisitiza.
Kwa upande wa Mwalimu wa Shule ya Msingi Isugile, Michael Kobelo amempongeza Mkuu huyo wa Idara kwa kuwa na klinini za kusikiliza na kutatua kero za watumishi jambo ambalo hapo awali halikuwahi kufanyika.
"Sisi watumishi tunajisikia faraja kwa sababu Idara yako mwanzo tuliiona ni kituo cha polisi kwa kutokua na mapokezi ya dhati lakini sasa kila mmoja anakubali ushirikiano uliopo, hongera sana," amepongeza.
================/


\

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa