• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

BARAZA LA MADIWANI LARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MBALIMBALI IGUNGA

Tarehe iliyowekwa: January 31st, 2025

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Mhe. Lucas Bugota amesema Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameleta fedha nyingi ambazo zimekua zikitekeleza miradi ya maendeleo katika sekta za maji, afya, elimu, umeme na miundombinu.

Mhe. Bugota aliyasema hayo Jumatano Januari 29, 2025 wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA) Meneja wa Wilaya – TARURA, Aswile Mwasaga aliishukuru serikali kwa kuwapa nyongeza ya bajeti kwa lengo la kuboresha miundombinu ya barabara.

Aidha, aliweka wazi kuwa Igunga inakilometa 19.185 za barabara za kiwango cha lami, kilometa 376.39 barabara za kiwango cha changarawe, kilometa 819.079 kiwango cha udongo, Madaraja 29, Drift na Makalvati 371.

Katika hatua nyingine, Taarifa ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kupitia Meneja wa Wilaya hiyo, Mhandisi Raphael Ambonisye ilidokeza kuwa vijiji 119 vimefikiwa na umeme.

Iliweka wazi kuwa inatekeleza mradi unaofadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kupeleka umeme kwenye vitongoji 3,060 huku ikikadiriwa kutumia takribani sh. bilioni 2.691 ambapo Mkandarasi amekwisha kamilisha kazi ya kukagua (Survey) na anaendelea na kuhamasisha (Mobilazation)  na Procurement (Manunuzi) kwa lengo la kuanza kazi ya kujenga laini.

Kwa upande wa Taarifa ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini (IGUWASA) kupitia Kaimu Mkurugenzi Mtendaji – IGUWASA, Mhandisi Bakari Mohamed ilibainisha kuwa huduma ya kupata maji  ni nzuri na inakidhi katika eneo lote ambalo IGUWASA inahudumia.

Pia, ilieleza kuwa Mtandao wa kusambaza maji umeongezeka katika maeneo ya pembezoni mwa mji kutoka Bunjiri kuelekea kijiji cha Majengo kilometa 3.5, kufungua vitua vingine kijiji cha Mwalala kupitia upanuzi wa Mtandao wa maji kilometa 1.07 na kupanua huduma ya upatikanaji wa maji kilometa 4.8 kijiji cha Ikulamawe.

Nayo Taarifa ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kupitia Kaimu Meneja wa RUWASA wilaya hiyo, Mhandisi Johnbosco Basabwa ilieleza kuwa inatekeleza mradi wa uchimbaji wa visima 10 katika vijiji vya Ncheli, Kazima, Igumo, Igondela, Igoweko, Kityelo, Imenya, Mgazi, Nguvumoja na Ibole kwa gharama ya sh. Milioni 600.

Aidha, ilitaja mradi mwingine ni upanuzi wa mradi wa maji ya ziwa Victoria kutoka Ziba kwenda Nkinga awamu ya pili unagharimu sh. bilioni 2.114 na upanuzi wa mradi wa maji ya ziwa Victoria kutoka Nkinga kwenda Simbo unaogharimu sh. Bilioni 1.032.

===== //// ==== ///// ====



Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. DC. SAUDA MTONDOO AWATAKA MADIWANI KUTEMBEA KIFUA MBELE UTEKELEZAJI ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IGUNGA

    May 16, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO APIGA MARUFUKU KUWEKA MAJI, MAWE NA MCHANGA LAINI KWENYE PAMBA

    May 16, 2025
  • DED IGUNGA AWATAKA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI KUDUMISHA UADILIFU BUSARA NA HEKIMA KUWAHUDUMIA WANANCHI

    May 10, 2025
  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa