• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

HAMISI ANENA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU YAMEKAMILIKA IGUNGA

Tarehe iliyowekwa: October 27th, 2025

MSIMAMIZI wa Uchaguzi  wa Majimbo ya Igunga na Manonga wilayani Igunga mkoani Tabora, Ndug. Hamisi H.  Hamisi  amesema wapiga kura 273,076 wanatarajia kupiga kura ifikapo Oktoba 29, mwaka huu katika majimbo hayo.


Ndug. Hamisi ameeleza hayo leo jumapili Oktoba 26, 2025 katika ofisi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi iliyopo katika wilaya hiyo mjini Igunga.


Kwa mujibu wa kifungu cha 69, (1) cha sheria ya  uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Ndug. Hamisi amewatangazia wananchi waliojiandikisha katika Daftari la Kudumu la wapiga kura la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuwa uchaguzi utafanyika siku ya Jumatano Oktoba 29 mwaka huu.


Ameeleza  kuwa vituo vilivyotumika kuandikisha wapiga kura katika Daftari la Kudumu la Wapiga kura ndio vitatumika kupiga kura.


Ameweka wazi kuwa vituo vitafunguliwa saa moja asubuhi na kufungwa saa 10 jioni huku kwa upande wa vituo vilivyoko Magereza vitafunguliwa saa mbili asubuhi na kufungwa saa tisa alaasiri.


"Nitumie fursa hii kuwaomba na kuwakaribisha wananchi wote wa majimbo ya Igunga na Manonga kujitokeza kwa wingi siku ya tarehe 29, Oktoba 2025 kwa lengo la kupiga kura," ametoa wito.


Aidha, ameeleza katika majimbo hayo kuna jumla ya vituo vya kupigia kura 728 ambapo vyote vipo tayari kuhakikisha zoezi hilo linatimia kwa mafanikio yaliyokusudiwa.


Katika hatua nyingine, amedokeza kuwa wanaendelea na zoezi la kuwahamasisha wananchi kwa njia ya matangazo, matamasha na michezo kwa lengo la kuwakumbusha na kuwahimiza wananchi kujitokeza kupiga kura.


Amewahakikishia wananchi kuelekea Oktoba 29, mwaka huu wamejipanga vema kufanikisha zoezi la uchaguzi kwa ufanisi.


"Tumeishapokea vifaa vyote wa uchaguzi na vipo tayari na zoezi la kusambaza katika vituo limekamilika," amethibitisha.


Tanzania hufanya uchaguzi mkuu kila baada ya miaka mitano, hivyo zikiwa zimebaki siku takribani tatu wananchi watapiga kura kutimiza haki yao ya kikatiba.

===================/



Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • WAHI FURSA ZA UWEKEZAJI IGUNGA September 25, 2025
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • HAMISI ANENA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU YAMEKAMILIKA IGUNGA

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI UCHAGUZI MKUU NGAZI YA VITUO WAKO TAYARI

    October 27, 2025
  • IDARA YA UTAWA IGUNGA ASIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

    September 15, 2025
  • MENEJIMENTI YAAHIDI KUENDELEA KUIPAISHA IGUNGA KATIKA KILA SEKTA

    September 13, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa