• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

DC ATOA MAELEKEZO KWA WATENDAJI WA KATA, KWENYE KIKAO CHA LISHE KILICHOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA IGUNGA 01/11/2023

Tarehe iliyowekwa: November 2nd, 2023

Bw;Simon P. Malando,Afisa Tarafa ya Igunga ametoa maelekezo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya amewataka Watendaji wa Kata kuhakikisha wanashirikiana na Wananchi kuhakikisha Watoto wanapata chakula shuleni,Watendaji ambao wamefikia asilimia 83 ya utoaji chakula shuleni katika Kata zao,walipata nafasi ya kueleza mbinu walizotumia hadi kufanikiwa,mbinu pekee inayoleta mafanikio ni kufanya vikao na wananchi na kukubaliana kiasi cha kuchangia,pia Mchangiaji anaruhusiwa kutoa kidogokidogo kutokana na kipato hadi amalize kiwango kilichokubaliwa kwenyekikao.(Walisema Watendaji wa Kata)

Mikakati na maadhimio iliwekwa kuwa kila Kata viongozi wa Chama na Serikali waseme kauli moja kwa wananchi juu ya uchangiaji chakula cha watoto Shuleni.

Divisheni za Halmashauri zinzojishughulisha na mikakati ya kuhakikisha Jamii inakuwa na Lishe bora walitoa taarifa za mafanikio ya utendaji kazi katika robo ya kwanza 2023/2024,Halmashauri ya Igunga inaelewa umuhimi wa Lishe bora katika kujenga Jamii imara yenye kujenga Taifa Bora.Pia uongozi wa Halmashauri unaheshimu na kusimamia Mikataba ya Lishe iliowekwa baina ya viongozi,Mhe SAMIA SULUHU HASSAN Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunamshukuru kwa kulitilia mkazo mkubwa suala la Lishe katika Jamii zetu ili ziweze kuwa na afya njema na kutekeleza na kujenga familia zinyeafya imara.Halmashauri imejiwekea mikakati kupitia Divisheni ya kilimo,mifugo na Uvuvi ya kuhakikisha jamii inalima vyakula vya aina tofautitofauti ili kuwa na chakula bora.

  LISHE  DIVISHENI  YA KILIMO,

MIFUGO NA UVUVI.

Katika msimu wa kilimo wa 2023/2024 Wilaya ya Igunga imelenga kulima hekta 83,809 za mazao ya nafaka na mizizi zinazotarajiwa kuzalisha tani 289,315 ili kuhakikisha upatikanaji  wa Wanga, hekta 15,724  za mazao ya mikunde zinazotarajiwa kuzalisha tani 15,724 ili kuhakikisha upatikanaji wa Protini na   hekta 1,855 za mazao ya bustani ambazo zinatarajiwa kuzalisha jumla ya tani 6,647.9 ili kuhakikisha upatikanaji wa Vitamini

Hadi kufikia  Juni 2023 Jumla ya Hekta 69,312 za mazao ya nafaka na mizizi zilikuwa zimelimwa na kuzalisha Jumla ya Tani 134,902 za mazao ya nafaka na mizizi. Kwa upande wa zao la mikunde Jumla ya Ha 13,520  zilikuwa zimelimwa na kuzalisha Jumla ya Tani 8,091.3 za zao  la mikunde.

Hivyo ukilinganisha na mahitaji ya Tani 129,586.9 za nafaka  zinazohitajika kwa mwaka kutosheleza watu 546,204 waliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga, Wilaya ilikadiriwa kuwa na ziada  ya takribani Tani 5,315.1 za nafaka ghalani zilizozalishwa kwa msimu wa kilimo 2022/2023.

Jumla ya wakulima 1,328 wamepatiwa elimu ya kilimo cha Mbogamboga  ili kuhakikisha upatikanaji wa vitamini  itokanayo na mazao ya bustani. Kati ya hao wakulima 1,184 wamepata elimu kupitia siku ya wakulima Nanenane na wakulima 144 wamepata elimu kupitia njia mbalimbali za huduma za ugani.

KITENGO CHA LISHE

Jumla ya maeneo 93, maduka 74 ya vyakula,mashine 12 za kusaga na kukoboa nafaka na sehemu 6 za usindikaji wa mafuta yalikaguliwa.Watoto 14 (Me 8 na Ke 6) walipata  matibabu ya utapiamlo mkali.Kata zote 35  na vituo vya afya 65 vya Wilaya ya Igunga zilikusanywa na zinaendelea kuingizwa kwenye mfumo wa taarifa  wa IMES. Maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji duniani yalifanyika na elimu ya lishe juu ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama yalitolewa kwa wananchi wa kata ya Mwanzugi.

Usimamizi katika vituo vyote ulifanyika katika vituo 4 vya kulea watoto wadogo mchana.Tulifanikiwa kufanya jiko darasa katika vijijini 19 sawa na asilimia 95

LISHE – ELIMU MSINGI,

Shule  139  kati ya shule 139 za serikali  zilitoa uji/chakula cha mchana kwa wanafunzi shuleni,Pamoja na halingumu ya mavuno msimu iliyopita lakini wazazi baadhi wameahidi kutoa chakula shuleni ili watoto wapate hata uji wa asubuhi.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa