• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

UMMY Aagiza Viongozi wa Halmashauri Kuongeza Ukusanyaji Mapato

Tarehe iliyowekwa: June 13th, 2021

Serikali imewaagiza Watendaji wa Halmashauri nchini kuhakikisha wana kusanya mapato kwa kuzingatia sheria,taratibu na kanuni na kwamba fedha zote ziwekwe benki ndani ya saa 24.

Kauli hiyo imetolewa  wilayani Igunga  na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikaliza Mitaa (OR TAMISEMI) Ummy Mwalimu akizunguma na Madiwani na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga.

Waziri Ummy alisema Halmashauri ya Wilaya ya Igunga fedha inaonekana inapelekwa benki lakini mapato yanayoonekana ni kidogo kwa kuwa mifumo ya kukusanyia mapayo kwa njia ya kielektroniki haitumiki ipasavyo.

Aliongeza fedha nyingi zitumika kabla hazijaingia benki kutokana na kisingizio cha kuharibika kwa mashine za kukusanyia mapato au kutokuwepo kwa mapato kwenye baadhi ya maeneo.

“Watendaji zingatieni maelekezo ya Serikali, ya kukusanya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kutumia mifumo ya kielektroniki, kwa kuhakikisha mapato ya ndani yaliyokusanywa yanawasilishwa benki ndani ya saa 24 kabla hayajatumika” alisisitiza

Aliwataka Madiwani na  Kamatiya fedha kuhakikisha wanasimamia ipasavyo ukusanyaji wa mapato ili Halmashauri ya Wilaya ya Igunga iweze kuwa na fedha nyingi za kupeleka na kuboresha huduma mbalimbali kwa wananchi

Aidha, Waziri Ummy aliwatataka Viongozina Watendaji wote kudumisha ushirikiano ili waweze kutimiza  wajibu wao kusimamia mapato na matumizi ya fedha za Halmashauri  hiyo kuwa itasaidia kuweka sawa mahesabu ya fedha vizuri na kupunguza hoja za ukaguzi.

Katika hatua nyingine Ummy amewatakawazazi wenye watoto waliopata ufaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tanokwenye shule za Serikali hapa nchini ambao wanakusudia kuwapeleka katika Shulebinafsi kuhakikisha wanatoa taarifa mapema ili nafasi hizo wapewe wanafunziambao wamefaulu lakini hawakupata nafasi za kujiunga na shule za Serikali.

Alisema jumla ya wanafunzi 86,896wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano lakini wanafunzi wapatao 3,800wamekosa nafasi ya kujiunga na kidato cha tano kutokana na uhaba wa nafasihizo.

Ummy aliongeza itakuwa vema kama wazazi na walezi wa wanafunzi waliopata nafasi kwenye shule za Serikali lakini hawataki kuwapeleka watoto wao huko watoe taarifa ili wale waliokosa nafasi wapate kuendelea na masomo kidato cha tano.

Aidha, Waziri Ummy aliahidi kupelekafedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa bwalo la chakula katika shule ya sekondari Ziba ili kuondoa kero inayowakabili wanafunzi wa shule hiyo.

Kwa upande wa Mbunge wa jimbo la Manonga wilayani Igunga Seif Gulamali alisema jumla ya shule 15 za msingi na 13 za sekondari zimepatiwa fedha na Serikali kiasi cha shilingi milioni 807 ili kujenga miundombinu mbalimbali.

Alisema mapema mwaka ujao wa fedhawanatarajia kupokea shilingi milioni 700 kwa ajili ya kujenga shule yawasichana ambayo itakuwa imekamilika kwenye miundombinu yote.

Gulamali alitoa shukurani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanaia  Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wananchi kote nchini.  


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa