• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe |
Igunga District Council
Igunga District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Msingi Mkuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Utumishi na Utawala
      • Mazingira
      • Maji
      • Ujenzi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili, Ardhi na Mazingira
      • Uvuvi na Mifugo
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
      • Ugavi
    • Kata
      • Our Wards
  • Vivutio vya Uwekezaji
    • Vivutio Vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha Ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Utawala
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
      • UKIMWI
      • Kamati Ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Madiwani
      • Meeting With Chairperson
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkatati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Vituo vya Habari
    • Press Release
    • Video za Shughuli za Ofisi Kitaifa
    • Makitaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi

WANANCHI WATAKIWA KUCHANGAMIKIA MILIONI 392.5 ZINAZOKOPESHWA MWEZI JANUARI HADI MACHI 2025

Tarehe iliyowekwa: December 4th, 2024

WANUFAIKA wa mikopo itokanayo na asilimia 10 wameendelea kumshukuru na kumpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuirejesha tena kwa utaratibu ambao umetajwa kuwa na ufanisi na wenye uhakika wa kufuatilia wanufaika hao kwa lengo la kuhakakikisha wanarejesha fedha hizo.

Akizungumza katika hafla fupi ya kuvipatia mikopo ya sh milioni 107.5 Vikundi saba vilivyokidhi vigezo katika robo hii ya mwaka wa fedha katika ukumbi wa Maxwel, Mkuu wa Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Sauda Mtondoo amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake ya kuendelea kuwainua wananchi kiuchumi.

‘’Kipekee nimpongeze na kumshukru Rais wetu Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira ya dhati ya kuwainua watanzania wakiwemo wajasiriamali kiuchumi,’’ ameshukuru na kuongeza kuwa:

“Hakika kwa kutumia muongozo mpya wanajihakikishia kikundi kinachokopeshwa kitakua na uwezo wa kufanya biashara na kurejesha fedha zilizokopeshwa.”

Aidha, amewataka Wataalamu waendelee kutoa elimu kwa wananchi mambo gani ya msingi wanapaswa kuyazingatia kwa lengo la kuwa na sifa ya kukopesheka kwa sababu dhamira ya Rais Dk. Samia ni kuona fedha inayotengwa inakwenda kwa watu waliokidhi vigezo vya kupata mkopo.

Ameeleza hatua hiyo itasaidia Jamii kufanya shughuli za kujiongezea kipato na kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja jambo ambalo litachangia kukuza uchumi wa Halmashauri, Mkoa hadi Taifa.

Hata hivyo, amewaomba wananchi ambao wamepata mkopo kuwa waadilifu, waaminifu na kuwa mfano wa kurejesha fedha walioikopo kwa mujibu wa mikataba waliyokubaliana kwa lengo la kuwakopesha wananchi wengine watakaokua na sifa kama wao.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Bi. Selwa Abdalla Hamid amewataka wananchi ambao hawajaunda vikundi kujifunza kwa waliokwishaunda  kwa sababu fedha za kuwakopesha zipo na zinahitajika zifike kwa vinaja, wanawake na watu wenye mahitaji maalumu ambao ni wajasiriamali.

Pia, amewafahamisha kuwa fedha hizo ni mkopo ambao sharti lake ni kurudisha kwa lengo la kuhakikisha inawanufaisha wananchi wengine wenye sifa.

‘’Tukiitumia mikopo hii vizuri itawafaidisha wananchi wengi na kuinuka kiuchumi, hivyo sisi halmashauri tutaendelea kutenga fedha na kutimiza malengo ya Rais Dk. Samia ya kuwainua wananchi kiuchumi na wapate kipato chao cha halali,”amesisitiza.

Pia, amewatoa hofu wananchi ambao wamekosa mikopo awamu hii wasikate tamaa kwa sababu fedha ipo ya kutosha, hivyo watimize vigezo, masharti, kanuni na taratibu watapata tu.

‘’ Hata kama utakosa mara 10 rudi na kajirekebishe tena kwa sababu ukiwa na nia huenda mara ya 11 utapata mkopo, fedha zipo na tunatamani mfuko wetu ubakie ziro na fedha zote zije kwenu,’’ ameweka wazi.

Awali akiwasilisha taarifa fupi mbele ya Mkuu huyo wa wilaya, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa wilaya hiyo, John Tesha amesema utoaji wa mikopo ni endelevu na fedha inayotolewa katika robo husika ikibaki itahamishiwa karika robo inayofuata huku akionya kuwa kikundi kitakachochindwa kupeleka marejesho kwa wakati hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Naye mmoja wa wanufaika wa mikopo hiyo, Daniel Kulyama ametoa wito kwa wananchi wengine waombe mikopo hiyo iwainue katika biashara zao na kukua kiuchumi.

‘’Ninamiaka zaidi ya mitatu ninafuatilia  mkopo lakini awamu hii nimepata fedha za Halmashauri kupitia kundi la walemavu, hivyo ninawahamasisha wenzagu ambao wanajishughulisha na ujasiriamali waombe watapata na kuinua mitaji yao ikiwemo kukuza uchumi,” amesema.

=======












Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA II October 12, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III October 12, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI WA VIJIJI DARAJA III October 15, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • MHE. RC. PAUL MATIKO CHACHA NA MHE. DC. SAUDA MTONDOO WAICHANGAIA IGUNGA UNITED SH. MILIONI 1.8

    April 22, 2025
  • MHE. DC. SAUNDA MTONDOO KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WATAKAOWEKA UCHAFU KWENYE PAMBA

    April 22, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWAHAKIKISHIA WANANCHI KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZOTE KARIBU YAO IGUNGA

    March 12, 2025
  • WANAWAKE WAKUMBUSHWA UMUHIMU WAO DUNIANI

    March 09, 2025
  • View All

Video

Maadhimisho ya siku Wanawake Kata Simbo ya SIMBO wilayani Igunga.
Video Zaidi

Viungio vya haraka

  • Hotuba
  • Pakua Fomu
  • Zabuni
  • Matangazo ya kibiashara
  • Matukio

Kurasa zinazofanana

  • Watumishi Portal
  • Poralg
  • Public Service Management
  • Tabora Region Website
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Huduma

Hatimiliki@2017Halmashauri ya Wilaya ya Igunga. Haki zote zimehifadhiwa